TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Saturday, July 5, 2014

BEI ZA MAFUTA NA UMEME ZAPANDA MISRI

Bei za mafuta na umeme zilizopanda zimeanza kutekelezwa nchini Misri huku serikali ikianza kukata ruzuku yake mbali na kupunguza matumizi ya bajeti yake ili kufufua uchumi ulioathiriwa na mgogoro wa kisiasa wa miaka kadhaa.
Baadhi ya bei za mafuta zinadaiwa kupanda kwa asilimia 78 huku bei ya umeme ikipanda maradufu katika kipindi cha miaka mitano.
Kwa sasa serikali inauza umeme kwa nusu ya gharama ya uzalishaji wake.
Kukatika kwa umeme nchini Misri limekuwa jambo la kawaida na maafisa wanasema kuwa gharama ya juu ya ruzuku imelemaza ukarabati na upanuzi wa mitambo ya kuzalisha umeme.
Waandishi wanasema kuwa kupanda kwa bei ya umeme nchini humo ni hatua mojawapo ya serikali katika kile kinachotarajiwa kuwa marekebisho ya kisiasa kwa ruzuku zinazosimamia Mafuta,Uchukuzi,chakula na kilimo.(P.T)
Chanzo:BBC

No comments:

Post a Comment