TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Saturday, July 19, 2014

GAZA:Israel yaendeleza mashambulizi yake 

Wakimbizi wa Gaza
Maafisa wa Umoja wa mataifa katika eneo la Gaza wanasema kuwa idadi ya raia wa Palestina walioachwa bila makao na ambao kwa sasa wanatafuta makao kufuatia mashambulizi ya nchi kavu yanayotekelezwa na Israel sasa imeongezeka maradufu kutoka elfu ishirini na mbili hadi elfu arobaini.
Raia wengi wameelekea Magharibi mwa Gaza ili kutoroka mashambulizi ya Israel.
Baada ya utulivu siku ya ijumaa kuna ripoti kwamba mizingi ya israel imefanya mashambulizi mengine usiku kucha.
Zaidi ya raia 60 wa Palestina wakiwemo watoto tisa wanadaiwa kuuawa tangu kuanzishwa kwa oparesheni ya nchi kavu na hivyobasi kuongeza idadi ya watu waliouawa kufikia 300.
Jeshi la Israel linasema kuwa mwanajeshi mmoja wa Israel aliuawa siku ya ijumaa kufuatia ufyatulianaji wa risasi wa wenyewe kwa wenyewe.(P.T)

No comments:

Post a Comment