TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Sunday, September 2, 2012

JESHI LA WANANCHI TANZANIA LAAZIMISHA MIAKA 48 TANGU KUANZISHWA KWA JESHI HILO
 Maofisa wa Jeshi wakiwa wamekaa kuangalia maonesho mbali mbali yaliyokuwa yakiendelea uwanjani


Vijana wa Jeshi wakiwa katika Gwalide





































































































Baadhi ya wananchi wakiwa wanaonyesha maandamo makali, ambapo kikosi cha jeshi kilikwenda kutuliza fujo hizo (picha za chini utaona walivyojeruhiwa na kubebwa machela.


Raia amebebwa machela baada ya kupatiwa kipondo toka kwa wanajeshi wakati walipokatazwa kuandamana nao wakiwa wanaendelea na maandamoano yao.












































































JESHI LA WANANCHI limesema kwa sasa linakabilina na changamoto ya kupambana na adui wa Ughaidi na si wale maadui wa kuwasubilia mipakani kama ilivyokuwa kipindi cha miaka ya nyuma.
Hayo yalisema na Mkuu wa chuo cha mafunzo ya huduma na Utawala cha Kijeshi , Luten Kanali Machera Machera , wakati wa maadhimisho ya miaka 48 ya Jeshi la Wananchi tangu kuanzishwa yaliyofanyika Mjini Morogoro katika viwanja vya chuo hicho.
Alisema Jeshi linazidisha umakini zaidi katika kutoa mafunzo mbalimbali ili kukabiliana na changamoto zilizopo za ughaidi hapa nchi.
Kanali Machera Machera, alisema miaka ya nyuma jeshi lilikuwa likipambana na maadui wa mipakani ambao wanatoka nchi nyingine na kuvamia, lakini kipindi hiki adui anatoka ndani na si nje kama ilivyokuwa ikidhaniwa.
“Sasa adui yupo ndani kwani vitendo vya ughaidi vinafanywa hapahapa ndani , hali ambayo ni hatali kwani huwezi kutambua haraka pale anapotokea  sasa jeshi lipo imara sana na litaendelea kutoa mafunzo ili kujiimarisha zaidi”Alisema Kanali Machera.
Aidha katika maadhimisho hayo jeshi lilifanya huduma za kijamii kama kufanya usafi katika kituo cha afya  zahanati iliyopo Kinguruila, kutembelea hospitali ya mkoa na kutoa mchango wa damu na  kuwaona wagonjwa na kufanya usafi katika soko la Manspaa hiyo .
Pia michezo mbalimbali ya kijeshi ilioneshwa kama Gwaride, mpira wa miguu, mpira wa nyavu,kukumbiza kuku na kutuliza fujo za maandamo.

No comments:

Post a Comment