TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Tuesday, January 20, 2015

Mwaka mmoja umepita tangu afariki mtangazaji Komla Dumor, BBC imeandaa kumbukumbu hii.

W1_MH_896 
Mwaka mmoja umepita tangu afariki Komla Dumor, mmoja ya watangazaji maarufu sana wa kituo cha BBC, alikuwa akiendesha kipindi cha Focus on Africa.
Shirika la habari la BBC limetangaza kuandaa Tuzo kwa heshima ya mtangazaji huyo mwaka mmoja baada ya kifo chake kilichotokea January 18, 2014 London na kuzikwa January 22 nyumbani kwao Accra, Ghana.
Dumor alikuwa mwandishi na mtangazaji mwenye kipaji cha kipekee kutoka Ghana, huku akisifika Afrika na duniani kote kwa kufanya kazi kwa kujitolea ambapo alikuwa akitoa taswira tofauti kuhusu Afrika kwa dunia nzima.
Shirika la BBC limejitolea kuendeleza kazi ya Komla kwa kutangaza tuzo ya uandishi wa habari kwa heshima kama mwandishi mahiri, Tuzo  itakayokuwa ikitolewa kwa waandishi wenye kipaji cha hali ya juu.
Hizi ni picha za kumbukumbu ya mwaka mmoja iliyofanyika  January 18 nyumbani kwao, Accra Ghana.
1.1959116-620x330
1.1959111

No comments:

Post a Comment