TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Tuesday, January 20, 2015

Kuhusu ile ishu ya Wanafunzi kupigwa mabomu ya machozi Kenya, iko hapa kauli ya Rais Kenyatta

uhunye
Waziri wa usalama nchini Kenya, Joseph Nkaissery amewaomba radhi  wanafunzi wa shule ya msingi ya Lang’ata baada ya  kupigwa mabomu ya machozi jana walipoandamana kupinga kunyang’anywa kipande cha ardhi ambacho kilikuwa uwanja wao wa kuchezea.
Jana hata hawataki tusherehekee, tukicheza wanatupiga na rungu wanatuletea madogi”– Mwanafunzi.
0
Waziri wa usalama Kenya, Joseph Nkaissery.
Rais Uhuru Kenyatta amelaani tukio hilo na  kumtaka Waziri wa Ardhi,  Charity Ngilu na Mwenyekiti wa Tume ya Ardhi,  Mohammed Swazuri kuwajibika na kueleza kwanini walizembea, huku Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo pia kalaumiwa kwa kusindwa kuzuia watoto hao kujihusisha na vurugu.
Bado haijafahamika ni nani aliyehusika na ujenzi huo.

No comments:

Post a Comment