TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Friday, January 23, 2015

BALOZI SEIF ASHIRIKI HARAMBEE CHUO CHA CBE 

unnamed (50)
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ally Idd akikabidhi mchango wake wa shilingi milioni 3 kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Uongozi ya Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE), Prof. Mathew Luhanga (katikati) kusaidia uboreshaji wa miundombinu ya chuo hicho jana usiku wakati wa harambee maalum ya ukusanyaji wa fedha iliyofanyika Hotel ya Serena jijini Dar es salamm.Kulia ni Mkuu wa Chuo hicho
unnamed (51)
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ally Idd na viongozi wa Chuo cha CBE wakitoa mkono wa shukrani kwa wadau mbalimbali waliotoa michango yao wakati wa harambee ya kuchangia maendeleo ya chuo cha CBE jana usiku jijini Dar es salaam wakati wa kilele cha maadhimisho ya miaka 50 ya chuo hicho .
unnamed (52)
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ally Idd akisoma majumuisho ya michango na ahadi zilizotolewa na wadau mbalimbali waliohudhuria harambee ya kuchangia maendeleo ya Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) jana usiku jijini Dar es salaam. Kiasi cha shilingi milioni mia tano arobaini, laki nane na elfu ishrini na tisa (540,829,000/=) zikiwa ni ahadi na fedha taslimu zilikusanywa.

No comments:

Post a Comment