TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Monday, August 11, 2014

JK AOMBWA KUSITISHA BUNGE LA KATIBA 

BungeKatibaz_aa762.jpg
JUKWAA la Katiba Tanzania (Jukata), limemuomba Rais Jakaya Kikwete asitishe Bunge Maalumu la Katiba, lakini pia limevionya vyama vya siasa nchini kuhusiana na vitisho vya kuwashughulikia wanachama wao kuhusiana na Bunge hilo.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa jana, Mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba Tanzania, Deus Kibamba, alisema kauli ya baadhi ya viongozi wa vyama vya siasa kwamba watawashughulikia wanachama wao, ambao ni wajumbe wa Bunge hilo si nzuri na kusisitiza kwa hali ilivyo sasa kuna haja Rais Kikwete asitishe Bunge Maalumu la Katiba.(MM)
"Yatosha tu kusema kwa sasa nchi imegawanyika vibaya kuhusu mchakato wa Katiba mpya na ulipofikia, haikuwa mshangao kushuhudia wajumbe watatu kutoka kundi la Ukawa (Umoja wa Katiba ya Wananchi) wakitinga bungeni na kujiandikisha ili kuendelea na vikao vya Bunge, akiwemo Mwatuka (Clara) kutoka CUF.
"Wengine ni waheshimiwa Leticia Nyerere, John Shibuda na Said Arfi, wote kutoka Chadema na Chiku Abwao pia wa Chadema, ambaye baada ya kusoma upepo kuwa Ukawa wamesusia kiukwelikweli amekanusha na kwamba alikuwa na shughuli zake binafsi mjini Dodoma na wala hakufika kushiriki vikao vya Bunge.
"Vyama vyao vya CUF na Chadema vimeahidi kuwachukulia hatua za kinidhamu kwa kukiuka maamuzi ya vikao halali vya kichama, lakini jambo moja dhahiri ni kuwa hawa ni wahanga tu wa tatizo kubwa zaidi la mpasuko wa kitaifa," alisema Kibamba.
Alisisitiza kuwa suala la kuchukuliana hatua au kushughulikiana si zuri na halileti tatizo la ufumbuzi uliopo kwani hata Ukawa wenyewe wamegawanyika, CCM nao wamegawanyika na jambo la msingi ni kutafuta ufumbuzi wa kitaifa kwani kuna mpasuko mkubwa ndani ya Bunge Maalum la Katiba, kijamii na hakuna maridhiano ya kitaifa.
"Kuna wajumbe wamechelewa kufika Dodoma kwa kuwa wanaamini Bunge Maalumu halipaswi kuendelea kwa hali hii, aidha hata miongoni mwa wajumbe wa CCM kuna mpasuko wa waziwazi kati ya wanaoamini kuwa Bunge Maalumu halipaswi kuendelea kwa sasa kwa kuwa theluthi mbili haitaweza kufikia maridhiano yanayohitajika ili Katiba mpya iweze kuandikika," alisema.
Alisema kuna wajumbe zaidi ya wanne wa CCM wametoa sauti kuhusiana na Bunge hilo na kwamba wapo wengi na ni ishara kuwa CCM nako kuna mpasuko.
Alidai kuwa CCM imegawanyika katika makundi matatu kuhusiana na mchakato huo na kuyataja kuwa ni kundi la wanaoondoka madarakani, kundi la wasio na upande ambao wapo kimya na kundi la wanaotaka madaraka.
"Pia hata miongoni mwa wana Ukawa kumetokea mpasuko kati ya wale wanaoamini kuwa hakuna haja ya kushiriki Bunge Maalumu, ambalo hatima yake hakutazaliwa Katiba mpya na wale wanaoamini kuwa wana haki ya kimsingi ya kushiriki vikao Bunge Maalumu la Katiba na kupata posho zao kama wale wa CCM," alisema.
Pia alieleza kuwa kuna wajumbe 201 walioteuliwa na Rais Jakaya Kikwete ambao wameduwaa na hawajui la kufanya.
"Tunashauri kuwa mchakato wa kuandika Katiba mpya uahirishwe hadi baada ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 ili uanze tena Januari 2016 na kwamba ili kuokoa gharama za uchaguzi wa Serikali za Mitaa, chaguzi hizi mbili zifanyike siku hiyo hiyo moja ya Uchaguzi Mkuu," alisema.
Pia Kibamba alieleza kitendo cha Ukawa kushindwa kurejea bungeni kinaunyima mchakato wa Katiba uhalali wa kisiasa na kisheria na kwamba upande wa wajumbe wa Zanzibar wanafanya kukosekana kwa theluthi mbili inayohitajika. 
CHANZO:HABARILEO

No comments:

Post a Comment