TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Tuesday, August 19, 2014

CHELSEA YAANZA LIGI KUU KWA KUIKANDAMIZA BURNLEY 3-1  1408395163253_lc_galleryImage_Chelsea_s_Ivorian_striker

Tembo: Didier Drogba akipiga shuti kujaribu kufunga goli baada ya kuingia katika dakika za lala salama 
MBWATUKAJI Jose Mourinho ameanza ligi kuu England ‘Swafii’ kabisa baada ya kufanikiwa kuingoza ugenini Chelsea kupata ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya timu mpya ya Burnley.
Wenyeji ndio walikuwa wa kwanza kuandika bao la kuongoza katika dakika ya 15 kupitia kwa Scott Arfield,  lakini mshambuliaji mpya wa Chelsea, Diego Costa alifungua akaunti ya mabao katika mechi za ligi kuu baada ya kuifungia timu yake bao la kusawazisha katika dakika ya 17.

Akaunti ya magoli: Diego Costa akifunga bao lake la kwanza la ligi kuu 
 Wakati Burnley wakiwa na matumaini ya kuongeza bao, Mjerumani, Andre Schurrle aliifungia Chelsea bao la kuongoza katika dakika 21 na Branislav Ivanovic akahitimisha karamu ya mabao katika dakika ya 34.
Tatizo kubwa kwa Burnley ni kwamba wachezaji wake hawajawahi kukutana na kitu kama hiki, hivyo kujikuta wakizidiwa maarifa kimbinu na kiufundi.

Hadi beki yumo: Ivanovic akifunga goli la tatu
Mabingiwa hao wa The Championship, mara kwa mara waliambiwa ligi ni ngumu lakini sio ngumu kama hivi leo.(P.T)
Katika mechi ya leo, Didier Drogba alianzia benchi na kucheza mechi ya kwanza tangu arudi Chelsea, lakini alishawahi kucheza mechi ya kwanza kabisa miaka ya nyuma.
Mlinda mlango, Thibaut Courtois naye alimkalisha kwenye ‘gogo; mkongwe Petr Cech.

 Mambo kutoka kwa Mjerumani: Andre Schurrle akiifungia Chelsea bao la pili
 Kikosi cha Burnley: Heaton, Trippier, Duff, Shackell, Mee, Taylor (Kightly 70), Marney, Jones, Arfield, Ings (Sordell 82), Jutkiewicz (Barnes 70).
Wachezaji wa akiba: Wallace, Gilks, Long, Dummigan.
Kadi ya njano: Sordell.
 Kikosi cha Chelsea: Courtois, Ivanovic, Cahill, Terry, Azpilicueta, Fabregas, Matic, Schurrle (Willian 78), Oscar (Mikel 82), Hazard (Drogba 84), Costa.
Wachezaji wa akiba: Cech, Luis, Zouma, Torres.
Kadi ya njano: Costa.
Mwamuzi: Michael Oliver (Northumberland)
Chanzo: http://shaffihdauda.com

No comments:

Post a Comment