WAKATI SSERENKUMA AKITUA, SIMBA KUSAINI BEKI WA KATI KUSUKA SIMBA MPYA

Na Baraka Mbolembole,
Wakati 
kiungo raia wa Uganda, Danny Sserenkuma akitaraji kutua nchini Jumatano 
hii kujiunga na Simba SC, Suleimani Matola ambaye ni kocha msaidizi wa 
mabingwa hao mara 19 wa kihistoria wa Tanzania Bara amesema kuwa timu 
yake ilimuhitaji zaidi kiungo Mkenya, Paul Kiongera lakini kutokuwa na 
uhakika wa urejeo wake uwanjani wanalazimika kuweka mbinu zao kwa 
Sserenkuma wakati huu wakihitaji kurudisha ubingwa wa ligi ambao mara ya
 mwisho waliutwaa msimu wa 2011/12.
Matola 
amesema kuwa Simba inatakiwa kumsajili mlinzi wa kati licha ya 
kumpandisha kutoka kikosi pili kijana,, Hassan . Simba ilihitaji 
kiungo-mbunifu katika eneo lake la mbele, Sserenkuma mwenye kasi, 
chenga, mpigaji hodari wa mipira iliyokufa, mfungaji makini, ni mchezaji
 mwenye maarifa mengi binafsi ambaye wakati mwingine anaweza kuibeba 
timu nzima katika mabega yake na kuipatia matokeo.(P.T)
Usajili 
wa dirisha kubwa ulifanywa kwa pupa, haukukidhi mahitaji muhimu ya 
nafasi lakini hilo linaweza ‘ kusahihishwa’ vizuri na usajili huu mdogo,
 na Matola amekiri wazi kuwa Sserenkuma ni chaguo ambalo Simba 
walilitaka. Uwepo wa Emmanuel Okwi, Amis Tambwe na Sserenkuma unaileta ‘
 Simba Mpya katika msimu uleule’. Ushindi mara moja katika michezo saba 
ya mwanzo msimu huu ni matokeo mabaya.
Lakini 
faida kubwa kwa Simba ni kwamba timu za juu nazo hazikuwa na matokeo 
bora kuliko. Simba wapo nyuma kwa pointi tano dhidi ya viongozi Mtibwa 
Sugar. Kufunga mabao ilikuwa tatizo, lakini pia safu ya ulinzi ilikuwa 
na ‘ matobo’ ambayo yameruhusu mabao sita. Ni mechi mbili tu ambazo 
Simba haijaruhusu bao ( Yanga SC 0-0 Simba SC, Simba 1-0 Ruvu Shooting),
 wamefunga mabao saba katika michezo saba, ila hawajafunga katika mchezo
 mmoja tu.
Hii ni 
dalili na ubora wa timu, lakini katika ligi yenye mabadiliko ya kimbinu 
na ufundi, wachezaji kama Sserenkuma ni wa lazima kwa timu yenye malengo
 makubwa. Kuelekea mchezo wa hisani ‘ Nani Mtani Jembe-2′ kati ya Simba 
na Yanga wiki ijayo, Simba hawatajali sana matokeo, ila hawatapenda 
kufungwa na mahasimu wao, watatazama vizuri uwiano wa kiuchezaji kati ya
 idara na idara, kiucheza
TAMBWE, OKWI, SSERENKUMA,
Ni mfumo 
gani ambao utawapanga ‘ nyota watatu wa kimataifa’ katika safu ya 
mashambulizi?. Nani ambaye atafurahi kuona Tambwe akizungukwa na Okwi 
akitokea upande wa kushoto, Sserenkuma akitokea upande wa kulia na guu 
lake la kushoto?. Wakati wa kilele cha mafanikio ya FC Barcelona barani 
Ulaya, David Villa, Pedro Rodriguez na Leo Messi walitengeneza utatu wa 
hatari katika safu ya mashambulizi, hii ndiyo safu ya mashambulizi 
iliyomtetemesha, Sir Alex Ferguson pale Wembley, Mei, 2011 katika 
fainali ya mabingwa ulaya.

Katikati 
ya uwanja walikuwa na ‘ pass-masters, Xavi Hernandez, Andres Iniesta 
ambao walisaidiwa katika ukabaji na kijana mahiri katika upokonyaji wa 
mipira na kuanzisha pasi sahihi kwa wenzake, Sergio Busquets. Kila mtu 
wa soka anakumbuka kuhusu ubora wa ‘ Barca ya Pep Guardiola’ katika 
mfumo wa 4-3-3. Je, Patrick Phiri anaweza ku-copy na ku-paste na 
kuifanya Simba kucheza huru na kupata matokeo katika mfumo ambao 
ulimpatia mafanikio makubwa Pep?.
Phiri 
anaweza sababu alishafanikiwa kwa matumizi Ya mfumo huo. Ujanja wa Okwi 
katika ufungaji na utengenezaji wa nafasi za mabao kwa wenzake. Okwi 
amefunga mabao matatu msimu huu, Tambwe amefunga bao moja, wakati Danny 
anatua akiwa na tuzo ya ufungaji bora kutoka KPL. Itashangaza kama Simba
 wataendelea kufunga kwa ku-bahatisha mara baada ya ujio wa Sserenkuma.
ndiyo 
kwenye soka, majina makubwa si kigezo cha ushindi, lakini mafanikio 
binafsi ya Tambwe, Okwi na Sserenkuma yanawatambulisha kama wachezaji 
bora kutoka nje ya nchi ambao wapo katika ligi kuu ya Tanzania Bara. 
Utulivu, uvumilivu, u-tayari, uwajibikaji ni baadhi ya mambo muhimu 
ambayo wachezaji wanatakiwa kuwa nayo, ata mashabiki, wanachama na 
viongozi wa klabu.
Kilicho 
muhimu zaidi ni mbinu za mwalimu na namna wachezaji wake watakavyoweza 
kuchukua mafunzo kutoka katika viwanja vya mazoezi na kwenda nayo katika
 michezo rasmi huku wakiwafanya kwa kiwango kisichopungua asilimia 
70-65.
Chanzo:http://shaffihdauda.co.tz/
No comments:
Post a Comment