Ndege ya KDF yaanguka Somalia

Ndege ya jeshi la KDF nchini Kenya imeanguka katika eneo la Kismayu nchini Somali.
Ndege 
hiyo ilianguka siku ya Alhamisi mwendo wa saa tisa na robo ilipokuwa 
ikirudi Kenya baada ya kutekeleza mashambulizi katika eneo la Jamaame 
kusini mwa Somalia.
Kulingana
 na msemaji wa Jeshi kanali david Obonyo: ''Ndege ya KDF iliokuwa 
ikirudi nchini Kenya baada ya kufanya mashambulizi katika eneo la 
Jamaame kusini mwa Somali,ilikumbwa na matatizo ya kiufundi na kuanguka 
katika eneo la Kismayu .
Kanali Obonyo hata hivyo hakusema iwapo kulikuwa na majeruhi yoyote.
Jeshi la 
Kenya limesema kuwa ndege hiyo ilianguka kutokana na hitilafu za 
kimitambo baada ya kufanya oparesheni katika eneo la Jamaane Kusini mwa 
Somalia.
Hata 
hivyo baadhi ya mitandaoa iliyohusishwa na kundi la AL shabaab 
imechapisha habari kuwa AL shabaab wamedai kuwa ndio waliodungua ndege 
hiyo mwendo wa saa tisa Alasiri, Afrika Mashariki.
Msemaji 
wa kiksoi cha kivita cha Al shabaab Sheikh Abdi Azizi Abu Musab 
amenukuliwa akisema kuwa walishambulia ndege hiyo kwa kombora baada ya 
kulipua kijiji cha Bulaguduud.
Kwa 
mujibu wa mwandishi wa BBC wa idhaa ya kisomali, ni vigumu kwa Al 
Shabaab kufanya shambulio kama hilo katika mji wa Kismayu kwa kuwa eneo 
hilo zima limefurika vikosi vya usalama vya AMISOM.
Mnamo 
mwaka wa 2012, majeshi ya Kenya yaliuteka mji wa bandari wa Kismayu, 
unaotazamiwa kuwa mji muhimu sana wa kiuchumi katika eneo zima la 
Somalia kutoka kwa wanamgombo hao wa Al shabaab.CHANZO:BBC
No comments:
Post a Comment