Maamuzi ya Rais Kenyatta kwa Mawaziri wake kufuatia kuendelea kwa mashambulizi ya kigaidi Kenya
Baada ya nchi hiyo kuelemewa na 
mashambulizi mara kwa mara na shinikizo la wananchi Rais Uhuru Kenyatta 
amemwachisha kazi  Waziri wa Usalama Joseph Ole Lenku na kumteua Waziri mpya wa Usalama Joseph Nkaiseri, kuchukua nafasi hiyo huku  Inspekta Jenerali wa Polisi David Kimaiyo akilazimishwa kuachia ngazi.
Baada ya lile shambulio la siku kumi 
zilizopita ambapo kundi la Al Shabaab liliwaua abiria 28 waliokuwa 
wanasafiri kwa basi kutoka Mjini Mandera karibu na mpaka wa Somalia, 
Kimaiyo na Ole Lenku wamekuwa wakikabiliwa na shinikizo za kujiuzulu 
kufuatia kukithiri kwa mashambulizi ya kigaidi na kuhatarisha  usalama, 
ambapo jana Novemba 02 wachimba kokoto 36 wameuawa na kikundi cha Al 
Shaabab katika kaunti ya Mandera.
“… 
Hapa ni mahali tukemekaa kama mimi mwenyewe nimekaa miaka tisa ile mambo
 nashuhudia saa hii sijawahi jionea na macho yangu watu kuuliwa sijawahi
 ona, by the way maisha yetu iko hatarini…”
“...Nakimbilia
 usalama wangu juu nahofia pale kwa nyumba hujui watavamia lini 
 watakuja lini, saa ndio natoka kwangu kwa nyumba nakaa nakuja kukaa 
hapa kulingana na ile mazingira tunayo  nakaa hapa kupata ulinzi wa 
Serikali inakuwa ni ngumu sana, sisi ndio tunafanya msituni tulio eneo 
la hapa Mandera Town wavamivi wanavyokuja wanapita njia za misituni sasa
 Polisi kujua ni ngumu…”
Rais Kenyatta amesema kuwa baada ya mazungumzo na Kimaiyo alikubali kustaafu mapema kwa sababu zake binafsi.

No comments:
Post a Comment