Hollande ziarani Kazakhstan

Rais wa 
Ufaransa, François Hollande, amejielekeza KazakhstanIjumaa Desemba 5, 
ili kuimarisha uchumi na biashara kati ya nchi hizo mbili.
Na RFI
Ni ziara 
ya tatu ya rais wa Ufaransa nchini Kazakhstan tangu kutangazwa uhuru wa 
taifa hilo mwaka 1991. François Mitterrand na Nicolas Sarkozy marais wa 
zamani wa Ufaransa walifanya ziara ya kikazi nchi Kazakhstan kabla ya 
François Hollande.
Rais 
Hollande amewasili nchini Kazakhstan Ijumaa Desemba 5 mapema asubuhi, 
kwa ziara ya saa 48, ambapo lengo ni kuimarisha uchumi na biashara kati 
ya Ufaransa na nchi hiyo yenye nguvu katika ukanda wa Asia ya Kati.(P.T)
Kazakhstan
 ni nchi tajiri kutokana na rasilimali za madini hususan madini ya 
uranium, kwani ni ya kwanza kwa kuzalisha madini hayo ulimwenguni. 
Kazakhstan inazungukwa na rasilimali kama chuma, makaa ya mawe, dhahabu,
 fedha na kadhalika. Fedha zinazotokana na mauzo ya dhahabu nyeusi nje 
ya nchi inawakilisha peke yake zaidi ya nusu ya mapato ya serikaliya 
Kazakhstan.
Kazakhstan
 ni nchi jirani ya mataifa yenye nguvu ambayo ni Urusi na China. 
Makampuni mengi barani Ulaya yameendelea baada ya nchi zao kuanzisha 
bishashara na Kazakhstan.
Kwa sasa Ufaransa inachukua nafasi ya tanu katika masuala ya biashara, huku Italia ikiongoza kwa kuchukua nafasi ya kwanza.
Ufaransa 
inawakilishwa nchini Kazakhstan na kampuni ya mafuta Total, ambayo ni 
mshirika wa kampuni ya gesi ya Kashagan, aidha Areva, kampuni 
inayoendesha shughuli zake katika migodi ya Uranium kusini mwa nchi. 
Kazakhstan ni nchi ya kwanza kwa kuitolea Ufaransa kiwango kikubwa cha 
uranium.
Hata 
hivyo Ufaransa inaiuzia Kazakhstan helikopta na silaha nyingi. Ziara 
hiyo ya rais Hollande nchini Kazakhstan ina manufaa makubwa kwa uchumi 
wa Ufaransa. Rais Hollande ameshirikiana katika ziara hiyo na ujumbe 
mkubwa wa matajiri wa makampuni makubwa nchini Ufaransa kama EDF, GDF, 
Veolia, Airbus, Peugeot pamoja na Vinci.
Hayo yakijiri Kazakhstan imekua ikinyooshewa kidole na mashirika ya haki za binadamu kwa ukiukwaji wa haki za binadamu.
No comments:
Post a Comment