Sing'atuki ng'o:Mugabe

Rais Robert Mugabe awalaumu baadhi ya wapinzani wake ndani ya chama cha ZANU PF kwa kupanga kumuondoa mamlakani.
Rais wa 
Zimbabwe Robert Mugabe amelaumu baadhi ya watu ndani ya chama chake 
tawala cha ZANU-PF kwamba wanapanga kumng'oa madarakani.
Akizungumza
 katika kongamano la chama hicho, Mugabe amesema amebaini kuwepo 
majaribio ya kuwahonga wajumbe kumpinga kama kiongozi, lakini 
akasisitiza wajumbe hawawezi kupokea hongo.
Mugabe 
ameahidi kupambana na rushwa ndani ya chama na kukabiliana na maafisa wa
 chama hicho ambao kazi yao ni kutoa hongo na kupokea rushwa.BBC

Wanachama wengi wa chama hicho wangali ni wafuasi sugu wa Rais Mugabe
Hasira ya
 Mugabe ilionekana kufuatia madai ya njama ya kutaka kumuua yanayodaiwa 
kuandaliwa na naibu wake Joyce Mujuru. Hata hivyo Mujuru alikanusha 
madai hayo ambayo yamekuwa yakimuandamana.
Mugabe alisema kutokuwepo kwa Bi Mujuru kwenye mkutano huo wa chama kunaonyesha kuwa anaogopa.
Kadhalika Mugabe amesema Mujuru ni mwizi anayepanga kumuondoa mamlakani kwa kushirikiana na maafisa wengine wa chama.

Maelfu ya wajumbe wa chama walihudhuria kongamano hilo mjini Harare
Chama 
tawala cha Zimbabwe kinakumbwa na vita vya ndani kwa ndani kuhusiana na 
nani atarithi nafasi ya Mugabe ambaye ana miaka 91 na ambaye ameongoza 
tangu uhuru wa taifa hilo.
Hata hivyo amekanusha madai ya kwamba anataka kujiuzuru na kusema kuwa huo ni upuuzi.
Hivi 
karibuni afisa mwingine mkuu wa chama tawala, Robert Gumbo aliiambia BBC
 kwamba Mugabe mwenye umri wa miaka 90 amegeuza chama tawala na 
kukifanya kama mali yake binafsi.

Bi Joyce Mujuru amedaiwa kupanga njama ya kumuua Mugabe ili achukue mamlaka kutokla kwake.
Gumbo alisema lengo kuu la Mugabe ilikuwa kuendeleza uongozi wa chama kwa niaba ya mke wake Grace.
Bi Mujuru
 ambaye amekanusha madai hayo alionekana kama mtu ambaye anechukua 
usukani wa chama kutoka kwa Mugabe ambaye walipigania naye uhuru wa nchi
 hiyo kutoka mikononi mwa watwala wazungu.
No comments:
Post a Comment