TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Friday, August 7, 2015

Tanzania yazidi kuporomoka viwango vya kimataifa vya FIFA

FIFAAAA
Timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, imezidi kushuka katika viwango vya ubora wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) na sasa imeshuka kwa nafasi moja zaidi na kushika nafasi ya 140.
Orodha hiyo imetolewa jana na Shirikisho la soka duniani FIFA na imeonyesha kuwa, Tanzania ndiyo nchi inayoshika nafasi ya chini zaidi katika Ukanda wa Afrika Mashariki ambapo Uganda inashika nafasi ya 74, huku Kenya ikiwa ya 116.
Algeria ndiyo inayoongoza kwa Afrika kwa kushika nafasi ya 19 ikifuatiwa na Ivory Coast inayoshika nafasi ya 21.
Timu zinazoongoza katika nafasi 10 bora ni; Argentina, Ubelgiji, Ujerumani, Colombia, Brazil, Ureno, Romania, England, Wales na Chile.

No comments:

Post a Comment