TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Thursday, August 13, 2015

Leo nimepita kwenye hili soko la Samaki, takwimu na idadi ya wafanyabiashara hizi hapa

.
.
Kazi yangu ni kuhakikisha nakusogezea kila stori inayonifikia na leo nimepita Feli Dar es Salaam ambapo ni eneo linalohusika na shughuli za uvuvi wa Samaki.
Inawezekana ukawa ni mpenzi wa chakula cha Samaki lakini haufahamu kinatoka sehemu gani na ndio sababu kubwa iliyonifanya nije hapa kwenye hili soko kuu ili nikusogezea kila ambacho haukifahamu.
.
.
Baada ya kufika kwenye soko hilo nimefanikiwa kumpata Mwenyekiti wa soko Ally Kibwana ambaye ameelezea namna ya uvuvi wa samaki pamoja na idadi ya wafanya biashara katika eneo hilo.
.
.
‘Kwa muda wa kawaida samaki kuwapata tunapata tani milioni moja kwa siku kutokana na kuingia kwa samaki sehemu mbalimbali Mafia, Kilwa na wavuvi wetu wa hapa wanaoenda na kurudi kwa hiyo kutokana na hali ya bahari kubadilika kutokana na tabia ya nchi kuna upepo mkali ambao umesababisha samaki kidogo kupungua kwa hiyo hatufiki kile kiwango tunachokihitaji’ – Ally Kibwana
.
.
‘Kazi moja ngumu ya Uvuvi  kwasababu mfano uvuvi wa madagaa tunatumia nyavu na kuna uvuvi ambao tunatumia boti hizi ndogo tunazihitaji ngwanda ni kutupa nyavu kutega ukishatega halafu watu wanashuka chini  kuzisukuma zile nyavu ili kupata samaki lakini ni moja kati ya kazi ngumu kwasababu bado tuna uvuvi wetu wa kizamani  hatujapata uvuvi wa kisasa kama tulivyoahidiwa na Serikali’ – Ally Kibwana
.
.
‘Wafanyabiashara waliopo hapa feli wanakaribia elfu kumi  sasa hivi walipo sokoni kwasababu tupo katika kata kuna zone namba 1 mpaka namba 8, zone 8 ambayo inashughulika  kuvua na  kurudisha mali na kuja kuuza zone namba 1, toilet hapa ziko mbili ambao zinauwezo wa kuingiza  mara moja watu kumi lakini hazitoshi kwasababbu watu ni wengi  tathmini ya mwanzo ilikuwa ni watu  elfu 10000 ila kwasasa wamezidi yaani idadi imeongeza’ – Ally Kibwana.
.
.
.
.
.
.
.

No comments:

Post a Comment