Burundi: hali ya wasiwasi yatanda Bujumbura

Pierre-Claver
 Mbonimpa, mwanaharakati wa haki za binadamu nchini Burundi, alizuiliwa 
jela kwa zaidi ya miezi minne. Hapa ni wakati alipokua Mahakamani 
akisubiri kusikilizwa, Julai 4 mwaka 2014.
Na RFI
Mwanaharakati
 wa haki za binadamu akiwa pia kiongozi wa shirika linalotetea haki za 
binadamu na za wafungwa APRODH, Pierre-Claver Mbonimpa ameponea kuuawa 
baada ya kujeruhiwa kwa risasi alizovyatuliwa na mtu aliyekuwa kwenye 
pikipiki katika kata ya Kanga wilayani Kinama, Kaskazini mwa jiji la 
Bujumbura.
Hali ya wasiwasi imetanda katika mji wa Bujumbura na wakaazi wa mji huo wameingiliwa na hofu baada ya kusikia tukio hilo.
Uvumi wa 
kuuawa kwa Pierre-Claver Mbonimpa ulianza kuzagaa tangu Jumapili Agost 2
 nchini Burundi. Lakini Jumatatu mchana wiki hii, mwanaharakati huyo 
amekanusha taarifa hiyo.
Saa 
zisiozidi nne baadae, yaani saa 12 na robo, mtu aliye kuwa kwenye 
pikipiki amemfyatulia risasi Pierre-Claver Mbonimpa wakati alipokua 
akirudi nyubani katika kata ya Carama wilayani Kinama, Kaskazini mwa 
jiji la Bujumbura.(P.T)
Pacifique
 Nininahazwe, mmoja kati ya wanaharakati wa mashirika ya kiraia akiwa 
pia kiongozi wa muungano wa mashirika ya kiraia FOCODE, yanayopinga 
muhula wa tatu wa Pierre Nkurunziza, ametoa wito wa kuzidisha ulinza 
katika hospitali ya Polyclinique Centrale de Bujumbura anakolazwa 
Pierre-Claver Mbonimpa, akisema anahofu huenda mwanaharakati huyo 
akamaliziwa maisha.
Balozi wa
 Marekani amewasili katika hospitali anakolazwa Pierre-Claver Mbonimpa, 
huku akielezea masikitiko yake kuona mauaji yamekua sugu nchini Burundi,
 hususan katika mji mkuu wa Bujumbura.
Hayo 
yanajiri wakati hali ya wasiwasi imetanda mjini Bujumbura na katika 
vitongoji vyake. Hali hii inatokea wakati katika hotuba yake Jumapili 
jioni baada ya kifo cha mkuu wa zamani wa Idara ya Ujasusi, jenerali 
Adolphe Nshimirimana mapema jumapili asubuhi, rais wa Burundi Pierre 
Nkurunziza aliwatolea wito raia kuwa watulivu na kujizuia na chochote 
kile ambacho kinaweza kuchochea chuki na machafuko.
Hata 
hivyo milio ya risasi imeendelea kusikika Jumatatu jioni wiki hii katika
 wilaya ziliyokuwa za waandamanaji hususan Nyakabiga, Cibitoke na Bwiza.
 Mpaka sasa haijajulikana hasara iliotokea.
Jumapili 
asubuhi afisa mwengine wa Idara ya Ujasusi wilayani Musaga, aliuawa 
nyumbani kwake na watu wasiojulikana. Mauaji yamekithiri nchini Burundi,
 ambapo mauaji yamekua yakishuhudiwa kila kukicha
No comments:
Post a Comment