TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Saturday, December 28, 2013

Wanajeshi wa Somalia wauawa kwa Bomu

Takriban wanajeshi watano na afisa wa jeshi wameuawa katika mlipuko wa bomu mjini Mogadishu,nchini Somalia mashuhuda wameeleza.
Mlipuko huo unaelezwa kutokea wakati wanajeshi hao wakipata malipo yao nje kidogo ya mji huo.
Sababu ya mlipuko huo haijafahamika,majeruhi kadhaa wamepelekwa hospitalini kwa matibabu.
Wanamgambo wa kiislamu, al Shabab walitimuliwa kwa nguvu mjini Mogadishu mwaka 2011 lakini wameendelea kufanya mashambulizi nchini humo
Kundi hilo lenye uhusiano na kundi la kigaidi la al -Qaeda linadhibiti maeneo kadhaa katikati ya Somalia.(P.T)

No comments:

Post a Comment