SUDAN KUSINI YATIBUA JARIBIO LA MAPINDUZI

Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir, 
anasema vikosi vyake vimefanikiwa kutibua jaribio la mapinduzi, baada ya
 usiku mzima wa mapigano katika mji mkuu wa nchi hiyo Juba.
Bw. Kiir, anayetoka katika kabila 
kubwa zaidi la wa Dinka amewatupia lawama wanajeshi wanaomtii aliyekuwa 
makamu wake Riek Machar, anayetoka katika kabila dogo la Nuer.
Aidha Kiir ametangaza amri ya kutotembea usiku mjini Juba na kusema serikali sasa inaudhibiti mji huo.
Makundi hasimu ya wanajeshi walipigana
 vikali kwa saa kadhaa na kuna ripoti za kuwepo majeruhi maelfu 
wakiripotiwa kukimbilia usalama wao.
Milio ya risasi sasa inaripotiwa 
kupungua. Kumekuwa na hali tete ya kisiasa nchini Sudan Kusini tangu 
mwezi Julai wakati Rais Kiir alipovunja na kuwafuta kazi mawaziri wote 
katika baraza lake akiwemo Makamu wa Rais Bw.Machar.(P.T)
No comments:
Post a Comment