MACHAR: SIHUSIKI NA JARIBIO LA MAPINDUZI

Aliyekuwa makamu wa Rais wa Sudan 
Kusini Riek Machar aliyekimbilia mafichoni amekataa madai kuwa amehusika
 katika jaribio la mapinduzi.
Ameiambia BBC kuwa wa kulaumiwa kwa 
machafuko yaliyotokea katika mji mkuu wa Juba ni rais Salva Kiir ambaye 
anadai kuhusika kwake.
Machar 
ambae alifarakana na Rais Salva Kiir mnamo mwezi wa Julai alimshtumu kwa
 "kuchochea mapigano ya kikabilai" ili kuficha udhaifu wake..
Rais Kiir amesema kikundi cha 
wanajeshi wanaomuunga mkono Bwana Machar kilijaribu kutwaa madaraka kwa 
nguvu usiku wa Jumaapili lakini walishindwa.
Alisema mapigano hayo yalianza pale 
watu waliovalia mavazi ya kijeshi walipofyatua risasi katika mkuano wa 
chama kinachotawala cha (SPLM).
Lakini Bw Machar aliiambia BBC: "Hakukuwepo jaribio lolote la mapinduzi."
Lakini Bw Machar aliiambia BBC: "Hakukuwepo jaribio lolote la mapinduzi."
Rais wa baraza la usalama la umoja wa 
mataifa Gerard Arud amesema kuwa mzozo unaoendelea nchini Sudan Kusini 
ambao umechukua mrengo wa kikabila unaweza kugeuka na kuwa vita vya 
wenyewe kwa wenyewe.
Bwana Arud ameiambia BBC kwamba umoja 
wa mataifa umepata habari kwamba mamia ya watu tayari wamepoteza maisha 
yao tangia jaribio la mapinduzi lifanyike siku ya jumapili,ijapokuwa 
amesisitiza kuwa sio raia wanaolengwa.
Ameiambia BBC kwamba takriban raia 
elfu 20 wamepewa hifadhi katika makao ya umoja wa mataifa katika mji wa 
Juba na kwamba wanakumbwa na uhaba wa chakula na madawa.(P.T)
No comments:
Post a Comment