FURSA: MAFUNZO YA KUPIGA ALA ZA MUZIKI

Action 
Music Tanzania (AMTZ) inatangaza fursa kwa watu wote kujiunga na mafunzo
 ya kupiga ala za muziki yanayoanza desemba 19 mwaka huu, lengo likiwa 
ni kuwajengea uwezo wanamuziki wa kupiga ala na kufanya maonesho kwa 
weledi na utaalamu zaidi.
Mafunzo 
yanayotolewa ni pamoja na upigaji wa ala za muziki zikiwemo gita, 
kinanda, tarumbeta, saxophone, konga, drum set, na upigaji wa ngoma za 
asili. Pia yatatolewa mafunzo ya ‘body percussion’ yaani matumizi ya 
mwili katika kutengeneza midundo ya muziki. 
Mafunzo 
hayo yanafanyika kwenye ofisi za AMTZ zilizopo maeneo ya Mwenge karibu 
na magorofa ya jeshi ambapo ili kujiunga na mafunzo haya wasiliana nao 
kwa simu namba 0686928828 au barua pepe, actionmusictz@yahoo.com, Like Facebook Page au tembelea www.amtz.org(P.T)
 Mwalimu Abeid Mussa akitoa maelekezo ya wakati wa mazoezi ya kufanya onyesho la muziki 
 Mwalimu wa Kinanda Prosper Shirima (katikati) akifundisha
Mwalimu wa Gita, Ashimba (kushoto) akitoa maelekezo ya namna ya kupiga chombo hicho
No comments:
Post a Comment