HII NDIO TAARIFA RASMI YA KUFUKUZWA KOCHA WA YANGA ERNST BRANDTS

Uongozi wa klabu ya Young Africans SC 
umempatia taarifa (Notice) ya siku ya thelathini (30) kocha mkuu 
mholanzi Ernie Brandts juu ya kusitisha mkataba wake kuanzia jana 
Disemba 22 mwaka huu.
Maamuzi hayo yanafuatia muenendo wa 
matokeo mabaya katika michezo iliyopita ya Ligi Kuu, kirafiki na bonanza
 la Nani Mtani Jembe dhidi ya Simba SC mwishoni mwa wiki.
Hatua ya Young Africans SC kusitisha 
huduma na Brandts isichukuliwe kama chuki bali ni moja ya sehemu ya 
kuhakikisha tunaboresha benchi la ufundi ili tuweze kupata matokeo 
mazuri katika Mashindano yanayotukabili.
Ukitazama uwezo wa mchezaji mmoja 
mmoja wa Yanga SC na wapinzani wetu, na soka tulilocheza kwenye mchezo 
wa mwishoni mwa wiki kwa kweli ni dhahiri mwalimu amefikia mwisho 
kimbinu na hana njia mbadala.
Young Africans SC imekua ikicheza 
chini ya kiwango katika michezo ya Ligi Kuu hali iliyoplekea kupata 
ushindi kwa tabu na wakati mwingine timu kupoteza pointi.
Kufuatia kupewa taarifa ya siku 30, 
Brandts ataamua mwenyewe kama ataendelea kusimamia mazoezi ya timu au 
kuondoka moja kwa moja kabla ya muda huo ukiwa haujakamilika.(P.T)
            
Ikiwa Brandts ataondoka mapema timu 
itaendelea na mazoezi kama kawaida katika kila siku asubuhi katika 
uwanja wa bora kijitonyama kujiandaa na mzunguko wa pili wa Ligi Kuu na 
mashindano ya kimataifa chini ya kocha msaidizi Fred Felix "Minziro".
Ili kuhakikisha timu inafanya vizuri katika mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom na mashindano ya kimataifa uongozi unakamilisha maandalizi ya safari ya kambi nje ya nchi na taratibu zote zitakapokamilika tutawajulisha.
Aidha uongozi upo katika mchakato wa kumapata mrithi wa Brandts ambaye ataungana na timu kwa ajili ya maandalizi ya mzunguko wa pili na Mashindano ya klabu Bingwa Afrika.
Mwisho tunawaomba wanachama, wapenzi na washabiki wa Yanga wasivunjike moyo kufuatia matokeo ya bonanza mwishoni mwa wiki, uongozi unajipanga kuhakikisha timu inaimarika kwenye benchi la ufundi na kurudisha furaha katika mzunguko wa pili wa VPL.
Abdallah Bin Kleb
Mwenyekiti - Kamati ya Mashindano
Young Africans Sports Club.
DAR ES SALAAM
23 Disemba, 2013
                    
Ili kuhakikisha timu inafanya vizuri katika mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom na mashindano ya kimataifa uongozi unakamilisha maandalizi ya safari ya kambi nje ya nchi na taratibu zote zitakapokamilika tutawajulisha.
Aidha uongozi upo katika mchakato wa kumapata mrithi wa Brandts ambaye ataungana na timu kwa ajili ya maandalizi ya mzunguko wa pili na Mashindano ya klabu Bingwa Afrika.
Mwisho tunawaomba wanachama, wapenzi na washabiki wa Yanga wasivunjike moyo kufuatia matokeo ya bonanza mwishoni mwa wiki, uongozi unajipanga kuhakikisha timu inaimarika kwenye benchi la ufundi na kurudisha furaha katika mzunguko wa pili wa VPL.
Abdallah Bin Kleb
Mwenyekiti - Kamati ya Mashindano
Young Africans Sports Club.
DAR ES SALAAM
23 Disemba, 2013
No comments:
Post a Comment