TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Tuesday, February 25, 2014

JATA WAWAPATIA ZAWADI WANAFUNZI WALIOSHINDA KUANDIKA INSHA

Wanafunzi wakiwa wamekaa tayari kwa kupokea zawadi zao

Afisa elimu mkoa wa Dar es Salaam, ambaye ndiye aliyekuwa mgeni rasmi kwa kukabidhi zawadi hizo kwa wanafunzi walioshinda




Mwanafunzi huyu ndiye aliyekuwa wa kwanza apambo alipatiwa zawadi wa Lap top


Wanafunzi watano bora ambao walishinda wakipiga picha pamoja na wadhamini wao


SHIRIKA lilisilo la kiserikali toka Nchini Japan  JICA ALUMNI ASSOCIATION OF TANZANIA (JATA)  limetumia kiasi cha Dola 800 za Kimarekani  kutoa zawadi kwa wanafunzi wa shule za sekondali nchini  walioweza  kuandika  na kuisoma  insha iliyoandaliwa na  shirika hilo.
Insha hiyo iliyoandaliwa na JATA  ilikuwa inahusu “What are the role of public secondary school in changing of social economic environment in Tanzania” ambapo jumla ya wanafunzi zaidi ya 100 walishiriki  kutoka Tanzania Bara na Visiwani.
Katibu wa Shirika hilo  nchini DK. Zacharia Mganilwa alisema JATA kwa kushirikiana na JICA wamekuwa  wakiendesha miradi mbali mbali ya maendeleo ya elimu na kwa mwaka huu wanafunzi wa shule nyingi walikuwa na mwamko wa kushiriki zoezi hilo tofauti na mwaka jana ambapo shule sita tu zilizoshiriki. 
DK. Mganila alisema  lengo la shirikia hilo kuandaa insha hiyo ni kupima uelewa wa wanafunzi kwa kuwajengea misingi ya kujiamini  na kujituma katika masomo yao .
Aidha Afisa elimu wa Mkao wa Dar es Salaam, Bw. Kiduma Mageni , kwa sasa JICA imekuwa ikitoa msaada mkubwa wa kufadhili miradi mbali mbali nchini ikiwemo ya ujenzi na upande wa elimu kwa kuwasaidia kuwapeleka baadhi ya walimu nchini Japan na kuwapatia mafunzo.
“Baadhi ya walimu huwa wanakwenda nchini Japani kwa kupata mafunzo zaidi ili wanaporudi nchini watoe mafunzo bora kwa watoto kwa kiwango kinachotakiwa, Aidha pia wajani nao wamekuwa wakijitolea katika kufundisha masomo ya hisabati na Sayansi kwenye shule za sekondari hapa nchini” alisema Bw. Mageni.
Alisema mashindano hayo pia yameleta changamoto kubwa kwa wanafunzi na kuonekana na uelewa mzuri  na kuwajenga uwezo wa kujiamini hasa kwa watoto wa kike ambao ndio wanakuwa kinara wa kuongoza na kujizolea zawadi kibao,
Alisema Mwaka jana katika shindano hilo mshindi  wa kwanza alikuwa ni mwanafunzi wa kike Faiza Khanis Ussi wa kidato cha tatu kutoka shule ya Sunni Madressa toka Zanzibar kwa  kupata alama 81  ambapo alizawadiwa Laptop moja aina HP na Certificate .
Hali kadhalika mwaka huu pia mshindi wa kwanza ni mwanafunzi wa kike kutoka mkoa wa Kilimanjaro  shule ya secondary ya Oshara  ni Zusaz Mmari  wa kidato cha nne,alipata alama 90 ambapo amepatiwa Laptop  moja aina ya HP ,Certificate  na Dictionary mbili.
Wshindi wengine waliobahatika kupata zawadi zingine mbali mbali ni Samwel Steven  ambaye alikuwa mshindi wa pili toka shule ya Kilindi iliyopo Sanya Juu, Mariaum Ramadhani toka shule ya Lumumba toka Zanzibar,  Furaha Mika toka shule ya Malangali Mbeya, ambapo jumla ya wanafunzi kumi walioshinda walipatiwa zawadi zao.

No comments:

Post a Comment