Whatsapp yanunuliwa na Facebook, nini tutegemee 
            
Kama ulikuwa haufahamu, habari kuu 
katika ulimwengu wa Teknohama kwa siku ya leo ni Facebook kuinunua 
Whatsapp kwa bei ya dola bilioni 19.  Nunuzi
 hilo ni la programu pekee na siyo kampuni ingawa wafanyakazi wa 
whatsapp watajiunga na timu ya Facebook moja kwa moja, mission za 
whatsapp zitaendelea kubaki kama zilivyo, alieleza Jan Koum ambaye ni muanzilishi wa whatsapp.
Kwa wasio fahamu, whatsapp ni moja ya programu ya simu za mkononi 
inayokuwezesha kutuma ujumbe wa simu kupitia kwenye intaneti badala ya 
ujumbe mfupi (sms). Kwa kutumia whatsapp, inamaana utaepuka gharama za 
sms huku ikiwa imesheheni matumizi mengine mengi zaidi kama kutuma 
picha, sauti uliyojirekodi nk.
Hadi sasa, whatsapp ina watumiaji hai milioni 450 kila mwezi kutoka 
nchi nyingi duniani, huku kukiwa na watumiaji wapya zaidi ya milioni 
moja kila siku. Hivyo, ni dhahiri kuwa whatsapp ni programu pendwa na 
yenye kutumika.
 
                        
        
        
        
            
Whatsapp inaweza kutumika kama njia rahisi zaidi ya mawasiliano kwa watu binafsi na hata makampuni, 
Ingawa makampuni mengi ikiwemo 
Facebook yamekuwa yakitegemea huduma za matangazo kama njia ya kuingeza 
kipato, whatsapp ni programu ambayo, huwezi kuonana na matanagazo na 
wamejizatiti kuwa ni wataendelea hivyohivyo bila ya matangazo. Na pia 
whatsapp ni bure kwa kwa mwaka wa kwanza na huchaji $1 kwa mwaka kama 
gharama ya kujiunga kwa miaka inayofuata. Hivyo kabla ya Facbook 
kuinunua whatsapp ni dhahiri walishajipanga kwenye hili, kwani, hili 
ndilo linaloifanya whatsapp iwe tofauti.
Akielezea sababu ya kuinunua 
whatsapp, mwanzilishi wa Facebook alisema, wameinunua whatsapp kwa 
sababu whatsapp ina thamani. Na wao wakiwa kama wafanya biashara lengo 
lao kubwa ni kuongeza thamani ya biashara yao illi waendelee kuwa 
salama. Hivyo, wanaamini nunuzi la whatsapp litakuwa na tija na manufaa 
kwa wote, wanunuzi na walionunuliwa. Hivyo ubora na misingi ya huduma ya
 whatsapp utaendelea kuwa juu kama ilivyo sasa.
Lakini, dili hili la kuinunua whatsapp halikuja ghafla, bali limekuja
 kwa kuangalia muelekeo na mabadiliko ya watumiaji wa mtandao. Taarifa 
zinaonesha kuwa, asilimia zaidi ya 52% ya watumiaji wa mtandao kwa sasa 
ni wale wanaotumia simu. Na pia matumizi ya email kama njia ya 
mawasiliano yamezidi kupunguasiku hadi siku. Na siku zinavyozidi kwenda 
mbele inamaanisha idadi hii itakua.
Pia, kwenye uwanja wa ujasiriamali, unatakiwa kuishi kwa kuyachunga 
mazingra na siyo kuomba dua mambo yasibadilike, hivyo ununuzi huu 
umekuja ili kuhakikisha Facebook inakuwa na udhibiti wa mazingira ya 
watumia intaneti na mtandao.Kitendo cha Facebook kuinunua whatsapp, 
kinaiwezesha kujikita zaidi kwenye kundi kubwa la watumiaji wa intaneti 
ambao wengi ni vijana.
Kwakuwa watumiaji wengi wa whatsapp ni wa kwenye simu, na kwakuwa yao
 ni moja ya programu zenye mamilioni ya watumiaji, hivyo kuimiliki 
whatsapp inamaanisha kumiliki hisa kubwa kwenye soko la watumiaji hao. 
Na hii itaiweka Facebook katika hali ya kudhitibi soko. la intaneti na 
mitandao jamii. Facebook pia watapata njia wa kuwafikia watumiaji hawa 
moja kwa moja kama ilivyokuwa kwa instagram, hivyo hii ni moja nunuzi 
lenye faida kwao.
Watu wengi wamekuwa wakijiuliza, je kitendo za Facebook kuinunua 
whatsapp kina faida yoyote kwa kampuni? na nini sisi watumiaji wa 
whatsapp tutegemee? Kutokna na sababu nilizozitaja juu (thamani), hivyo 
ni yumkini kabisa, Facebook wanaweza kufanya kati ya vifuatavyo.
1. Kuiunganisha whatsapp moja kwa moja na Facebook.
Ikumbukwe kuwa, whatsapp itaendelea kuwa whatsapp, hivyo usifikiri 
kwamba kesho hakutakuwa na whatsapp bali watumiaji wote watapelekwa 
Facebook, la , ila whatsapp itakuwa na ushirikiano wa kiutendaji na 
Facebook na kuzifanya ziwe imara zaidi. Ila, ili whatsapp iunganishwe na
 facebook, ni dhahiri kuwa whatsapp lazima ifanyiwe maboresho na 
kuongezewa baadhi ya matumizi ambayo yataiwezesha kuiunganisha moja kwa 
moja na Facebook, isiishie kwenye mawasiliano tu. Kunatakiwa kuongezwe /
 boreshwa zaidi zile huduma ya kijamii.
Kwa
 mfano, tutegemee kuwa na uwezo wa kutuma visasisho(updates) ambavyo 
vitaonekana kwenye Facebook yako. Hii itaipe ya maisha yako hapohapo 
kwenye whatsapp. Hii itaipeleka whatsapp kufanana sana na moja ya 
mtandao unaofanya kazi zake kama whatsapp unaoitwa Wechat.Huu ni mtandao
 uliofanikiwa sana kwa China.
2. Kutafuta / alika marafiki wa facebook kwa kutumia namba za simu na siyo email pekee
 Facebook ilipoanza, ilikuwa inategmea sana email kama njia ya kutafuta 
marafiki, ila kadri siku zinavyozidi kwenda, matumizi ya email kama njia
 ya mawasiliano ya kawaida yamekuwa yakipungua, hivyo kutegemea email 
kunaiweka facebook kwenye kikomo cha kutanuka. Kwakuwa whatsapp inatumia
 namba za simu, na kwakuwa facebook imeinunua whatsapp, basi tutegemee 
kuwa kutakuwa na uwezo kwa watumiaji wa Facebook kuwaalika watu wajiunge
 na facebook kwa njia ya ujumbe wa simu, na hii itaunganishwa vyema kwa 
kutumia whatsapp.
3. Kuongezwa huduma zaidi ambazo ni za kulipia.
 
Kwakuwa lengo la kuwekeza ni kuongeza kipato.Iwe moja kwa moja au la, ni
 dhahiri kuwa facebook watakuja na njia zitakazowawezesha kuongeza 
kipato kwa kutumia whatsapp, hivyo kutakuwa na huduma zaidi ambazo si za
 lazima, ila kama utazihitaji, basi utatakiwa kulipia kiasi fulani. Hii 
ni moja ya njia zinazotumika kipindi unaandaa bando la huduma.
Hivyo,kwa watumiaji wa Facebook na Whatsapp, tutegee mambo mengi zaidi.