TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Saturday, August 18, 2012



WANANCHI WATAKIWA KUIBUA MIRADI YA MAENDELEO


Habari na Salma Mrisho, Geita
Wananchi wametakiwa kujua kwamba maendeleo hayawezi kuja bila wao kujitambua kuwa wana nafasi katika kushiriki na kutoa maoni katika kuibua miradi mbalimbali ya kijamii itakayowaletea maendeleo.
Hayo aliyasema Afisa mipango wilaya ya Geita mkoani Geita Bw Andrew Chikwanda alipokuwa akizungumza na mwandishi wa gazeti hili kuhusu uhusikaji wa wananchi katika uibuaji wa miradi.
Alisema kuwa wananchi,wadau na serikali ni watu wanaotegemeana katika shughuli mbalimbali hasa za kuibua miradi na kila mmoja kwa nafasi yake anatakiwa aisimamie kikamilifu ili matunda ya hiyo miradi ionekane.
“zamani serikali ilikuwa inatoa fedha na kuanzisha miradi lakini ilionekana ile miradi matokeo yake yalikuwa madogo na wakati mwingine ilikuwa haionekani  thamani ya miradi lakini kwa sasa wananchi wana nafasi ya kuibua miradi yao na wafanye hivyo”alisema Bw Chikwanda
Pia aliwataka wananchi kama walikuwa hawajui wana hiyo nafasi watambue na wakae katika vijiji vyao na waibue miradi ambapo inatakiwa ipitishwe na mkutano wa kijiji na mabaraza ya maendeleo ya kata na baada ya hapo wana kaa na madiwani na wataalamu kuijadili ipi ipewe kipaumbele kulingana na fedha iliyopo kwa mwaka husika.
Bw Chikwanda aliongeza kuwa miradi ya wananchi imekuwa na maendeleo kwa kuwa wao ndio waanzilishi na wanasimamia ipasavyo kuhakikisha inafanikiwa kuliko angefanya mtu mmoja ambapo ingeweza kuchukua muda kukamilika.
“unajua wananchi wajue kuwa wao ndio wahusika na wasisibiri ile ruzuku inayotolewa na serikali kupelekwa ngazi ya kijiji ndio ifanye kila kitu maendeleo yatachelewa sana waibue tu miradi sisi ni watekelezaji wa kufanikisha hilo”alisisitiza Bw Chikwanda
Aliongeza kuwa kuwa mara nyingi wanatembelea miradi iliyobuniwa na wananchi na kuangalia viwango vya ujenzi kama vinakidhi na wanatoa nyaraka kuwa kila hatua ya ujenzi ihakikishe nkuwa mhandisi ametoa  cheti  ili kuruhusu hatua nyingine iendelee.
Aidha aliwataka wakuu wa idara na ofisi ya ujenzi kutembelea miradi inayoanzishwa na kuoana thamani yake na hata kutoa ushauri kuliko kuacha miradi inaendelea na ikikamilika kuonekana kuna kasoro kwani kwa kufanya hivyo tutakuwa tunawaangusha wananchi kwa nguvu kazi zao walizotumia.

MWISHO

No comments:

Post a Comment