TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Wednesday, August 15, 2012


WANANCHI WA GEITA NA MATATIZO YA USAFIRI 

Habari na Salma Mrisho ,Geita .
Wananchi wametakiwa kuwa na subira katika mchakato unaoendelea wa kuhakikisha suala la usafiri linaboreshwa kuanzia mijini hadi vijijini.
Hayo yalisemwa na Mkuu wa Wilaya Manzie Mangochie  wakati wakizungumza na wadau mbalimbali mwishoni mwa wiki  juu ya kuboresha suala la usafiri wa abiria mkoani hapa.
Alisema kuwa wananchi walikuwa wanapata tabu juu ya usafiri hasa baada ya kupiga marufuku magari madogo aina ya michomoko iliyokuwa inabeba abiria wengi na ni kinyume cha sheria na kuongeza kuwa kwa sasa tatizo hilo limetatuliwa kwani wafanyabiashara wa  magari aina ya hiace wameyaleta kutoka mwanza  na yanatoa huduma ya usafiri.
“wananchi jamani muwe mnatupa taarifa sio mpaka ajali zitokee na kama kuna michomoko sehemu inafanya kazi mtujulishe sheria ichukue mkondo wake”alisema Manzie
Alisema kuwa kwa sasa wanajipanga ili waweze kuweka vituo kila eneo na ili Geita iendane na hadhi ya Mkoa kuliko ilivyo sasa usafiri wa baiskeli umekuwa mwingi na pikipiki na wataalamu wamepitia baadhi ya maeneo ambapo umbali wa mji kwa km 10 kuna ruti zishapangwa na kwa vigezo vya Sumatra nauli itakuwa shilingi 500.
Aidha aliwataka wananchi watoe taarifa juu ya madereva wanaovunja sheria barabarani ili kuzuia ajali zinazoweza kuepukika mkoani hapa.
Kwa upande wamkuu wa wa Kikosi Cha Barabarani Kamanda John Mfinanga aliwahakikishia wananchi kuwa watafatilia kwa karibu kero zote za usafiri na kuhakikisha magari hayajazi abiria wengi na sheria zinazingatiwa.

MWISHO

No comments:

Post a Comment