TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Friday, October 31, 2014

Kivumbi cha Ligi kuu England 


Golikipa Simon Mignolet wa timu ya Liverpool ashindwa kuupangua mpira.
Kitimtim cha ligi kuu ya England kitaendelea tena kesho wakati ambapo mashabiki wa soka nchini humo na duniani kote watapata nafasi ya kuzishuhudia timu zao zikitafuta pointi tatu muhimu.
Newcastle Utd wataikaribisha Liverpool katika mchezo ambao utarushwa moja kwa moja kupitia idhaa ya Kiswahili ya BBC majira ya saa tisa unusu kwa saa za Afrika Mashariki.
Arsenal wao wataikaribisha Burnley, huku Chelsea nayo wakiialika QPR. Everton watakuwa nyumbani kucheza Swansea City. Hull City wataikabili Southampton. Michezo mingine ni itakayochezwa siku hiyo ya kesho ni kati ya Leicester City watakapo kwaana na West Brom, Huku Stoke City watakapoikabili West Ham utd.BBC
Siku ya jumapili ni mpambano wa kukata na shoka ambapo Manchester United wataavaana na Manchester City mechi ambayo pia itatangazwa moja kwa moja na Idhaa ya Kiswahili ya BBC ,huku Tottenham watakapokwaana na Aston villa.

Taarifa nyingine kuhusiana kesi ya kuanguka kwa kanisa la T.B Joshua

Synagogue-Collapse-BellaNaija1
Serikali ya jimbo la Lagos Nigeria, imesema sehemu ya jengo lililoaanguka katika kanisa la Synagogue Church of All Nations, ambalo lilijengwa kwa ajili ya kufikia wageni lilijengwa bila kibali cha Serikali.
Kamishna anayesimamia mipango miji Lagos, Olutoyin Ayinde amesema uchunguzi uliofanywa na tume iliyoongozwa na Oyetade Komolafe umeonyesha hakuna kibali kilichotolewa na mamlaka hiyo kuidhinisha ujenzi wa jengo la ghorofa sita.
Amesema kibali kilichotolewa kilikuwa cha ujenzi wa jengo la kanisa ambalo ni ukubwa wa ghorofa tano pekee, na uchunguzi umebaini kibali hicho kilikiukwa kwa kujengwa ghorofa nane badala ya tano.
Anyinde amesema mamlaka hiyo imeagiza mamlaka ya anga kuchunguza juu ya ndege ambayo imedaiwa kuzunguka jengo hilo muda mfupi kabla ya jengo kuanguka.
tb-joshua 
Kesi hiyo inayosikilizwa mahakama kuu Lagos imeahirishwa mpaka Novemba 5 ambapo T.B Joshua atatoa ushahidi. Jengo hilo lilianguka Septemba 12 na kuua watu 116.

Wanne wafariki katika ajali ya ndege, watano majeruhi

Ajali ndege
Watu wanne wamefariki katika ajali ya ndege iliyotokea saa chache zilizopita baada ya ndege ndogo kugonga jengo la uwanja wa ndege na kuwaka moto.
Ndege hiyo iligonga jengo la uwanja wa Wichita, Kansas Marekani na kusababisha vifo vya watu wawili waliokuwemo ndani kufariki ikiwemo rubani wa ndege, na watu wengine waliofariki waliokuwa ndani ya jengo.
Majeruhi watano katika ajali hiyo walipelekwa hospitali, watatu waliruhusiwa kutoka huku wengine wawili wakiendelea kutibiwa.
Kikosi cha askari wa zimamoto walipambana na moto huo na kuuzima ndani ya muda mfupi, na baadhi ya barabara za ndege uwanjani hapo zilifungwa japo ajali hiyo haikuathiri ratiba za ndege kutua na kuruka.
Ndege hiyo ina uwezo wa kubeba watu 13 japo idadi ya watu waliokuwemo ndani ya ndege haijafahamika, uchunguzi unaendelea ili kubaini chanzo cha ajali hiyo pamoja na thamani ya vitu vilivyoathirika kutokana na ajali hiyo

Picha kumi za Ikulu zinazoongoza kwa matumizi mabaya ya fedha duniani

Kuna malalamiko mengi tumekuwa tukiyasikia kuhusu Ikulu za nchi kuhusishwa na ufujaji mkubwa ama matumizi mabaya ya fedha.
Hizi ni picha na orodha ya Ikulu tano zinazoongoza kwa matumizi makubwa zaidi ya fedha duniani.
New Turkish presidential palace in Ankara
No. 1- Jumba jipya la Ikulu ya Uturuki, liko katika jiji la Ankara na kwa sasa huenda likawa jumba kubwa zaidi kuliko Ikulu ya Marekani. Ujenzi wake umegharimu zaidi ya Dola Mil. 350.
Turkey's new Presidential Palace at night
Muonekano wa jumba jipya la Ikulu ya Uturuki wakati wa Usiku.
OLYMPUS DIGITAL CAMERA
No.2- White House, Ikulu ya Marekani. Ikulu hii iko Washington D.C, na imekuwa ikitumika kama Ikulu tangu mwaka 1800, Marekani ikiongozwa na rais John Adams.
White House Night
Muonekano wa White House wakati wa usiku.
Brazil Pres. Palace
No. 3- Planalto, Ikulu ya rais wa Brazil. Iko katika jiji la Brasilia. Imekuwa ikitumika kama Ikulu tangu mwaka 1960, wakati huo rais akiwa Oscar Niemeyer.
Brazil Night
Muonekano wa Planalto, Ikulu ya Brazil wakati wa usiku.
Grand_Kremlin_Palace-1
No. 4- Grand Kremlin, Ikulu ya Urusi iliyopo jijini Moscow. Imeanza kutumika kama Ikulu tangu mwaka 1849.
Moscow Night
Muonekano wa Grand Kremlin, Ikulu ya Urusi wakati wa usiku.
Taipei Pres Palace
No. 5- Jumba la Ikulu ya Taipei, Taiwan. Imekuwa ikitumika kama Ikulu tangu mwaka 1950.
Taiwan Usiku
Muonekano wa Jumba la Ikulu ya Taipei, Taiwan wakati wa usiku.

Bunge lachomwa moto pamoja na nyumba za wabunge, rais agoma kuachia madaraka

Burkina FA
Mbali na maafa makubwa yaliyojitokeza ikiwa ni pamoja na majengo ya bunge kuchomwa moto pamoja na nyumba za wabunge, rais aliye madarakani amegoma kuachia madaraka yake.
Blaise Compaore rais wa Burkina Faso aliyekaa madarakani kwa miaka 27 anatajwa kuwa mmoja wa marais waliokaa madarakani kwa kipindi kirefu zaidi na bado anasisitiza kuwa ana miezi 12 zaidi ya kuendelea kuwepo madarakani kabla ya kukabidhi madaraka kwa rais ajaye.
Ban Ki-moon anatarajiwa kuwasili nchini siku ya leo kwa ajili ya kutafuta suluhu ya machafuko hayo.
Chanzo cha machafuko hayo kinatajwa kuwa ni kitendo cha bunge kutaka kufanya mabadiliko ya katiba ambayo yangemfanya Blaise Compaore kubakia madarakani kwa kipindi kingine zaidi.
Taarifa zinasema jeshi limelazimika kuongoza nchi hiyo ili kurejesha utulivu.

Obama apingana na unyanyapaa wa magavana wa New York, New Jersey

Obama III
Rais Obama amekosoa baadhi ya sheria zilizowekwa na majimbo na nchi mbalimbali katika kukabiliana na ugonjwa wa Ebola.
Obama amekosoa kuhusiana na sheria ya kuweka karantini siku 21 manesi na madaktari waliotoka nchi za Afrika Magharibi kuhudumia wagonjwa wa Ebola kwa kusema kuwa sheria hiyo inawavunja moyo watu hao walioamua kujitolea maisha yao kwa kuwasaidia waathirika wa ugonjwa huo.
Rais huyo hakutaja majina ya majimbo wala nchi ambazo anazikosoa kwa sheria hizo kandamizi, lakini New York na New Jersey zilitangaza utaratibu huo ambao ulianza kutekelezwa mwanzo wa wiki hii hivyo inaonekana ujumbe wa Obama umelenga magavana wa majimbo hayo.
Kauli ya Obama huenda ikawa na tafsiri inayokosoa vilevile uamuzi uliofanywa na serikali ya Australia wa kuzuia kuingia nchini humo mtu yoyote anayetokea ukanda wa nchi za Afrika Magharibi ambazo zimeathiriwa zaidi na janga la ugonjwa huo.

Thursday, October 30, 2014

Nyingine kubwa ya leo, Daraja kutoka Zanzibar mpaka Dar

daraja
Unaweza ukadhani ni ndoto lakini hii ni habari ya kweli baada ya Hifadhi ya jamii NSSF kutangaza uwezekano wa kujengwa daraja la kihistoria zaidi litakalounganisha Dar es salaam na Zanzibar.
Uwepo wa daraja hilo unaweza kuwa ni neema kwa Watanzania wote na hata nchi za jirani kwani itarahisisha shughuli za kiuchumi na kibiashara kwa asilimia kubwa kwa kupunguza kero ya usafiri kwa wananchi.
Gazeti la HabariLEO liliripoti kuwa kwa sasa Shirika hilo lipo katika mazungumzo na wataalamu mbalimbali ili kuangalia uwezekano wa kujenga daraja hilo katika bandari ya Dar kwa upande wa Bara na Unguja kwa upande wa Visiwani.
Mkurugenzi mkuu wa NSSF Ramadhan Dau alisema ujenzi wa daraja hilo si ndoto bali ni ukweli na tayari wameanza mazungumzo ya awali ili kutimiza malengo yao.
Umbali kati ya Dar na Zanzibar ni kilimeta73.43 sawa na maili45.62 hivyo kuwepo na mradi huo ni jambo linalowezekana kwani kuna madaraja marefu zaidi duniani yanayounganisha upande mmoja wa bahari na mwingine.
Kwa sasa daraja refu zaidi duniani kote ni lile la Danyang-Kushan lililopo nchini China ambalo lina umbali wa kilometa 165 sawa na maili102.4 ambalo lilifunguliwa Juni mwaka2011.

Msiba mwingine wa mwigizaji Bongo Movie 2014.

Mzee Manento 
Wiki moja  baada ya kutokea kwa msiba wa mmoja wa wasanii wa TMK Wanaume Family YP na saa chache baadaye ukatokea msiba mwingine wa aliyekuwa msanii wa maigizo na vichekesho Sherry Mwana, leo Oktoba 30 umetokea msiba mwingine Bongo Movie.
Taarifa za awali zimeanza kusambaa kupitia watu mbalimbali maarufu Tanzania ambao wameaanza kuonyesha masikito yao akiwemo msanii Bob Junior kuhusu kifo cha mzee Manento ambaye inadaiwa amefariki jana usiku.

Hawa ndio mastaa wanaogombea Ubunge jimbo moja kupitia vyama tofauti

Bunge Naija 
Taarifa kuhusiana na mastaa mbali mbali ikiwemo wa muziki, filamu, na michezo kuingia katika headline zinazowangumzia kujihusisha na siasa sio taarifa ngeni kuzisikia, ambapo kwa sasa mastaa wa movie wanaingia kwenye headline nyingine ya wao kwa wao kugombea nafasi ya ubunge kwenye jimbo moja kupitia vyama tofauti.
Mastaa wa filamu kutoka Nigeria Bob Manuel Udokwu na Tony One Week Muonago wanaendelea kuzungumziwa sio kwa sababu wamejiingiza kwenye siasa, bali kinachozungumziwa ni kitendo cha wao kugombea nafasi hiyo katika jimbo moja kitu  ambacho kimeanza kuvutia hisia za watu wengi.
Actors
Bob Manuel Udokwu (kushoto) na Tony One Week, waigizaji wa Nollywood waliojitosa kugombea katika Jimbo la Anambra.
Bob Manuel Udokwu anagombea kupitia chama cha APGA na Tony One Week Muonagor anagombea kwa tiketi ya ACN katika jimbo moja la Anambra, Nigeria ambapo uchaguzi mkuu wa nchi hiyo unatarajiwa kufanyika katikati ya mwaka 2015, ambapo staa mwingine wa Nollywood ambaye alitangaza kujiingiza kugombea ubunge ni Desmond Elliot.

Kilichomkuta ‘aliyemdiss’ refa wa kike

Referee 
Makamu wa Rais wa shirikisho la mpira wa miguu kaunti ya Northumberland, Uingereza John Cummings amesimamishwa kwa kipindi cha miezi 4 kwa kosa la kumwambia mwamuzi wa kike kuwa sehemu anayopaswa kuwapo mwanamke ni jikoni na sio katika uwanja wa mpira wa miguu.
Cummings amemtolea kauli hiyo mwamuzi Lucy May, kwamba hawezi kuhimili kazi ya kuwa mwamuzi, na kuongeza kuwa katika maisha yake yote hakuwahi kuona mwanamke akichezesha mpira wa miguu.
Tume huru ya uratibu wa shirikisho la mpira wa miguu imesema kuwa Cumming amekiuka kanuni za mpira wa miguu za shirikisho hilo kwa kutumia lugha ya kukashifu na ubaguzi wa kijinsia.
Makamu huyo wa rais amekiri kuwa hakuwa anamaanisha kwenye kile alichokizungumza bali ilikuwa ni utani ambao huenda May hajauchukulia hivyo, japo chama hicho kimesema nafasi ipo wazi kwa refarii huyo kukata rufaa juu ya hukumu hiyo.
Hukumu aliyopewa refa huyo inaambata na adhabu ya faini ya paundi 250 na pia adhabu ya kuhudhuria mafunzo.
Mkurugenzi wa chama cha soka Northumberland, Clive Oliver amekemea kitendo hicho na kusema mpira wa miguu unajumuisha watu wote na hakuna ubaguzi wowote unaopaswa kuvumiliwa

Unafahamu kuna watu watatu waliotokea Liberia hawajulikani walipo? Isome taarifa hii

TZA MMOJA WA WALIO WASILI APOKELEWA JKIA
Wakenya tisa kati ya kumi na mbili waliokua wamekwama nchini Liberia tangu kulipuka kwa ugonjwa wa Ebola wamewasili usiku katika uwanja wa Jomo Kenyatta International Airport (JKIA)  Nairobi, Kenya.
“..Awali tulikua tunatarajia wakenya 150 kutoka Liberia lakini ni kumi na mbili pekee walioonesha dharura ya kusafiri kurudi nyumbani, na kama mnavyojionea tumewapokea tisa pekee na hatufahamu wengine watatu waliko..”– Waziri Macharia.
Katika idadi hiyo ya watu tisa ni pamoja na watoto wanne na watu wazima watano ambao walikuwa kwenye ndege iliyotokea Brussels na abiria wengine 69 na majira ya saa 5:30 usiku wa jana.
Kuhusiana na Wakenya wengine watatu kati ya kumi na mbili waliotarajiwa kuwasili siku ya jana bado haijafahamika wapi walipo.
Waziri amesema serikali ina mpango wa kuwasafirisha kuwarudisha nchini humo Wakenya wengine watano kutoka Sierra Leone hivi karibuni.
Waziri ametangaza rasmi kuwa iwapo kuna mtu yoyote atabainika kuwa na dalili za Ebola atawekwa karantini kwa siku 21 na wale wasio na dalili zozote wataruhusiwa kurejea majumbani mwao.
TZA WAKENYA WAWASILI KUTOKA LIBERIA

Uchungu wa wazazi hawa kwa watoto wao umefikia kiwango hiki

Wazazi Kulinda Shule 
Kuna ukweli kwenye msemo wa waswahili unaosema “uchungu wa mwana aujuaye mzazi”, na ndio maana stori nnayokuletea huenda ikawa ngeni na hujawahi kukutana nayo, lakini wazazi hawa wameonesha namna walivyo na uchungu kwa vitendo na sio maneno pekee.
Stori kutoka Kenya inahusu kitendo cha wazazi kuamua kujichukulia jukumu la ulinzi wa eneo la shule ili kukabiliana na vitendo vya uhalifu ambavyo vimekuwa vinajitokeza mara kwa mara katika maeneo hayo.
Kila jioni Esuruan Awet ni moja ya wazazi hao ambao hujiunga na kikundi cha askari Polisi wa akiba kwa lengo la kupiga doria eneo la shule ya msingi Nakatong’wa, Mashariki mwa Turkana huko Kenya.
Eneo la shule hiyo limekuwa likikabiliwa na matukio ya kuvamiwa mara kwa mara kitendo kilichowafanya wazazi hao kujiunga na kikosi hicho kukabiliana na uhalifu huo.

Huyu ndiye Rais wa kwanza mzungu ndani ya Afrika tangu kuisha ubaguzi wa rangi

Guy Scott
Guy Scott ambaye alikuwa makamu wa rais Zambia wakati wa utawala wa Michael Sata ametajwa kushika nafasi ya urais wa nchi hiyo kwa sasa mpaka pale ambapo ataapishwa mara baada ya kufanyika uchaguzi mkuu wa nchi hiyo.
Waziri wa ulinzi Zambia Edgar Lungu amesema maandalizi ya uchaguzi huo yataanza muda wowote ambapo katiba ya nchi hiyo inaagiza kufanyika uchaguzi wa Rais ndani ya siku 90 baada ya kufariki kwa aliyekuwa rais wa nchi hiyo.
Scott ameteuliwa kushika wadhifa huo ambapo hii itakuwa mara ya kwanza kwa rais mzungu kuongoza nchi ya Afrika tangu kuisha kwa kipindi cha ubaguzi wa rangi Afrika Kusini chini ya utawala wa FW de Klerk.
Kulikuwa na utata uliotokana na katiba ya Zambia kumruhusu Scott kushika wadhifa huo kwa sababu wazazi wake wanatokea Scottland, huku katiba hiyo ikitaja rais wa nchi hiyo ni lazima awe Mzambia kamili kwa maana ya kwamba wazazi wake wote wawili wanapaswa kuwa wamezaliwa nchini humo

Wednesday, October 29, 2014

Hii ndiyo taarifa iliyotolewa na FIFA kuhusiana na Ebola

Fifa-headquarters-007 
Shirikisho la soka Duniani FIFA limesema mashindano ya kombe la dunia la FIFA kwa ngazi ya vilabu yanayotarajiwa kufanyika mwezi Desemba mwaka huu yataendelea kama ilivyopanga, huku likisisitiza vilabu vyote kuhusiana na kuchukua tahadhari juu ya virusi vya Ebola pindi inapofanyika michuano hiyo ya kimataifa.
Kitendo cha baadhi ya nchi kukumbwa na janga la Ebola kuliibua maswali namna ambavyo michuano hiyo itawezekana kufanyika na pia juu ya usalama wa wachezaji hasa pale ambapo watalazimika kwenda kucheza mechi katika moja ya nchi ambayo iko kwenye ukanda ulioathirika na ugonjwa huo.
FIFA imewatoa wasi wasi kwa kutoa ushauri namna ambayo itasaidia kupunguza hatari ya kuenea kwa maambukizi ya ugonjwa huo.
Mbali ya mapendekezo yaliyotolewa na FIFA ya kufanya vipimo vya afya za wachezaji wa vilabu husika baada ya kurejea kutoka moja ya nchi ambayo iko katika ukanda ulioathiriwa na Ebola, na kushauri naadhi ya mechi ambao zilipangwa kufanyika Guinea, Sierra Leone na Liberia kuhamishiwa katika viwanja ambavyo vipo katika nchi zenye viwanja vyenye nafasi.
Mbali na FIFA kusisitiza kuwatenga haraka wachezaji watakaoonesha dalili za Ebola wakati ikifanyika michuano ya kimataifa, vile vile imewataka wachezaji kutoka nchi zilizoathirika kuwa na tahadhali kubwa kwa kupima afya zao.

Kilichoamuliwa na Mahakama kuhusu kesi ya Chid Benz ni hiki

CHID
Rapa kutoka La familia Ilala Chid Benz mchana wa October 28 amesimamishwa kizimbani katika mahakama ya hakimu mkazi Kisutu na kusomewa mashtaka yanayomkabili.
Mashtaka matatu yanayomkabili Chid Benz ni;-
  1. Kukutwa na madawa na vifaa vya kutayarishaji uvutaji wa madawa
  2.  Kusafirisha madawa ya kulevya
  3.  Utumiaji wa madawa ya kulevya
Kwa sasa Chidi Benz amerudishwa rumande hadi Novemba11 ambapo kesi yake itatajwa tena, kuhusu dhamana ya mshtakiwa mahakama imesema itakuwa wazi kwa masharti ya kuwa na wadhamini wawili wanaotambulika na jumla ya pesa taslim million 1.

Soma hapa alichokiagiza Zitto Kabwe kwa CAG na BoT leo

News Cover
Taarifa zilizotufikia hivi punde zimesema Kamati Ya Hesabu za Serikali (PAC) Tanzania imeagiza ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) pamoja na Benki Kuu ya Tanzania (BOT) kufanya ukaguzi wa mchakato wa ubinafsishaji wa iliyokuwa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC).
Taarifa hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Serikali Zitto Kabwe, kupitia ukurasa wake wa Instagram (@zittokabwe) dakika chache baada ya kumalizika kwa kikao alichokifanya na waandishi wa habari Dar es Salaam leo.
 Zitto IIZitto I

Monday, October 27, 2014

Viwango vya Fifa vinatupa ukweli tunaouficha

KATIKA siku za hivi karibuni vyombo vya habari hasa vya michezo vimepambwa na taarifa za Tanzania kupanda viwango vya soka kwa mujibu wa takwimu za Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa).
Habari hizo zimepokewa katika namna nzuri ya kuonyesha kwamba Tanzania imepiga hatua na hivyo jambo hilo kuonekana ni la kujivunia.
Si nia yetu kubeza wanaojivunia mafanikio hayo kwani ndio ukweli wenyewe hasa unapoviangalia viwango hivyo na kuvifananisha na vilivyopita.
Kwa mfano takwimu za Fifa za mwezi Septemba, zilionyesha kwamba Tanzania ilikuwa ya 115 na takwimu zilizotolewa mwezi huu zinaonyesha kwamba Tanzania sasa ni ya 110.
Wengi waliopata taarifa hizo walijifariji hasa baada ya kuona Tanzania imepiga hatua hiyo na kuizidi hata nchi ya Kenya ambayo kwa mujibu wa viwango hivyo inashika nafasi ya 116.(P.T)
Kwa kuziangalia takwimu hizo hizo utaona kwamba Kenya imepata pigo kwa kuporomoka kutoka nafasi ya 111 iliyokuwa mwezi uliopita hadi kufikia ya 116 iliyopo sasa.
Hata hivyo tungependa kutoa tahadhari kwamba pamoja na hatua tuliyoipiga kwa mujibu wa viwango hivyo lakini bado wadau wanatakiwa kuviangalia viwango hivyo kwa mapana zaidi jambo ambalo tunaamini litawafanya watafakari kwa kina.
Tunasema hivyo kwa sababu ukivichambua kwa kina viwango hivyo utaona kama Tanzania haijapiga hatua yoyote ya kutisha, badala yake imeendelea kupanda na kushuka.
Kuna usemi wa siku hizi uliozoeleka wa homa za msimu, si vibaya kulifananisha soka la Tanzania na homa za msimu kama utaamua kuvichambua viwango vya Fifa.
Unaizungumziaje nchi ambayo rekodi zilizotolewa na Fifa mwezi Agosti zilionyesha kwamba ilikuwa ya 110, Septemba ikawa ya 115, Oktoba ikarudi nafasi ya 110?
Je ni vibaya kuzingatia takwimu hizo na kuliona soka letu kuwa ni mfano wa homa za msimu. Hatulisemi hili kwa nia mbaya bali tunachotaka ni kuona wadau wanavitumia vizuri viwango hivi kwa kujichambua na si tu kujivunia kupanda.
Katika kipindi chote cha mwaka huu, wakati pekee ambao Tanzania ilionyesha matumaini kwa mujibu wa rekodi za Fifa ni mwezi Julai kwa kushika nafasi ya 106 wakati ambao jirani zetu Kenya walishika nafasi ya 95.
Mwezi Juni ripoti zilionyesha kwamba Tanzania ilikuwa ya 113, Mei 122, Aprili 122, Machi 117, Februari 116 na Januari 118.
Kwa mantiki hiyo tangu tuuanze mwaka 2014, Tanzania haijawahi kuwa miongoni mwa timu 100 bora kwa mujibu wa rekodi za Fifa jambo ambalo linatosha kutufanya tuukubali ukweli kwamba soka letu bado.
Katika viwango vya Fifa Tanzania mara zote inashindanishwa kati ya nchi 207, kati ya nchi hizo Tanzania inazishinda baadhi ya nchi ambazo hazijulikani katika ulimwengu wa soka na tuna hakika wapo Watanzania ambao hawajawahi hata kuzisikia.
Mfano nchi kama Macau, Anguilla, Bhutan, Visiwa vya Cayman, Visiwa vya Cook, Montserrat, Vanuatu, Guam, Belize na nyinginezo.
Tunachotaka kukisisitiza hapa ni kwamba tufurahie kupanda lakini tuukubali ukweli kwamba soka letu bado lina kazi ya kufanya ili walau tuwe chini ya timu 100 bora duniani na tudumu katika nafasi hizo si kupanda na kushuka.
Chanzo:Mwanaspoti

CHADEMA, CUF, NCCR MAGEUZI NA NLD VYATILIANA SAINI MAKUBALIANO YA USHIRIKIANO


Viongozi wa juu wa vyama vinne vya siasa nchini Tanzania vimeingia makubaliano ya ushirikiano wa shughuli mbalimbali za siasa hii leo na miongoni mwa mambo hayo ni kusimamisha wagombea wa pamoja katika uchaguzi wa Serikali za Mtaa na Uchaguzi Mkuu wa wabunge, madiwani, wawakilishi na Rais 2015. Kutoka kushoto ni James Mbatia wa NCCR-MAGEUZI, Prof Ibrahim Li[pumba wa chama cha Wananchi CUF, Freeman Mbowe wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na Dk. Emmanuel makaidi wa NLD wakionesha hati yao ya makubaliano waliyoisaini jana katika viwanja vya Jangwani Dar es Salaam 

Viongozi hao wakishangilia kuzaliwa kwa ushirikiano huo huku makatibu wao wakiwa wameketi. kwa kuangalia siani za makubaliano wa ushirikiano bofya soma zaidi. (P.T)

Wafuasi, wanachama, wa vyama vya siasa vinavyounda ukawa wakifuatilia mkutano huo ambao ulianza kwa kuimba wimbo wa Taifa huku wanachama hao wakiwa wamekaa jambo ambalo lilielezwa na viongozi wao kuwa uzalendo ni ndani ya moyo. Chini ndio mambo waliyokubaliana.



NAHODHA WA BAFANABAFANA AUAWA 



Nahodha ambaye pia ni golikipa wa timu ya soka ya taifa la Afrika kusini Senzo Meyiwa enzi za uhai wake.
Nahodha ambaye pia ni golikipa wa timu ya soka ya taifa la Afrika kusini Senzo Meyiwa amefariki dunia baada ya kupigwa risasi. Jeshi la polisi la nchi hiyo limesema.
Tukio hilo limeripotiwa kutokea katika nyumba ya mpenzi wake iliyopo katika mji wa Vosloorus kusini mwa Johannesburg.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 aliichezea klabu ya Orlando Pirates na alicheza mechi nne zilizopita za timu yake ya taifa katika mechi za kufuzu za fainali ya mataifa ya Afrika.
Jumamosi alikuwepo katika tukio la timu yake pindi waliposonga mbele katika nusu fainali ya ligi ya Afrika kusini.
Katika maelezo yake Jeshi la polisi la afrika kusini limesema kwamba Meyiwa ameripotiwa kufariki wakati akiwasili hospitalini. BBC

Msichana asimulia ya Boko Haram

Baadhi ya wasichana waliotekwa nyara
Ni miezi sita sasa baada ya wanamgambo wa kiislam wa kundi la Boko Haram kuwateka wanafunzi wasichana Zaidi ya 200 kaskazini mashariki mwa Nigeria, wasichana watatu ambao wametoroka wamezungumza katika mahojiano maalum na idhaa ya Kihausa ya BBC.
Tukio hili linakuja wakati serikali ya Nigeria ikiwa katika makubaliano ya kusimamisha mapigano dhidi ya Boko Haram hatua itakayo saidia kuwaachilia huru wasichana waliotekwa na kundi hilo .
'' nilikuwa nataka kurukia nje wakati msichana mwenzangu aliponikamata kwa nyuma na kusema watakupiga risasi kama utafanya hivyo. Nikasema, nini utofauti wataniua mimi hapa na kuacha maiti yangu ikusachukuliwa nilikuwa nalia na kuomba mpaka tulipoifikia kambini" Anasimulia msichana mmoja alitoroka mikononi mwa Boko Haram.(P.T)
Akizungumza katika mahojiano maalum na idhaa ya Kihausa ya BBC, Msichana huyu anakumbuka jinsi alivyokuwa nyuma ya Lori wakati wanapinaji wa Boko Haramu walipomteka yeye na wasichana wengine.
Zaidi ya wasichana 200 kati miongoni mwao walikuwa walitekwa lakini wale waliokimbia walibahatika kutoingia katika hofu kubwa kwenye mikono ya watekaji.
Shirika la kimataifa la kutetea haki za binaadam la Human Rights Watch limesema wanawake wanaoshikiliwa na kundi la Boko Haramu wamekuwa wakinyanyaswa, kubakwa na hata kulazimishwa kuolewa.
Katika ripoti mpya ya shirika hilo inasema Wanamgambo hao wa Kiislam wamewawateka wanawake Zaidi ya 500 na wasichana tangu mwaka 2009.
Serikali ya Nigeria hivi karibuni imetangaza makubaliano ya kusimamisha mapigano dhidi ya Boko Haram ambayo hatua itakayawafanya wanamgambo ho kuachilia huru wasichana wa hao waliotekwa huko Chibok.
Lakini Boko Haram wenyewe hawajawahi kuthibitisha makubaliano yoyote ya kusitisha mapigano na hakuna dalili zozote za kuachiwa kwa wasichana haohivi karibuni.
Lakini kwa wale waliobahatika kutoroka, matatizo ya kisaikolojia bado yanawasumbua..

BONDIA THOMAS MASHALI AJIFUA KUMKABILI MKENYA HENRY WANDERA 


Bondia Tomas Mashali  kushoto akijifua wakati wa mazoezi ya kujiandaa kupambana na Bondia Henry Wandera kutoka kenya novemba 1 katika ukumbi wa frends corner manzese, akisimamiwa na Kocha wa Mchezo wa Masumbwi kutoka Sweeden, Juma Ntuve (www.superdboxingcoach.blogspot.com(P.T)
Na Mwandishi Wetu
BON DIA Thomasi Mashali  yupo katika maandalizi mazito ya kumkabili bondia kutoka kenya Henry Wandera Novemba mosi katika ukumbi wa Frends Corner Manzese Dar es salaam
akizungumza wakati wa mazoezi yake juzi Mashali amesema kuwa yupo fiti wakati wowote yeye kufanya kazi hivyo aofii ata kiogo mpambano huo na kuwataka mashabiki wake waje waone anavyo mgalagaza vibaya sana siku hiyo mkenya Wandera
mbali na mpambano huo siku hiyo kutakuwa na mapambano mengine ya utangulizi yatakayo wakutanisha Mbayo Ilunga na Fred Sayuni wakati Joseph Mbowe ataoneshana umwamba na Saidy Salum na Ramadhani Johncena ataoneshana ubabe na Baina Mazola
na mipambano mingene mikali zaidi siku hiyo kutakuwa na michezo ya utangulizi zaidi ya nane yenye raundi sita sita katika mpambano huo siku hiyo kutakuwa na ulinzi wa kutosha kabisa kutokana na kujipanga vizuri katika swala hilo kingilio ni shilingi, 7000; kwa kila mtu mchezo huu utapambwa na burudani mbalimbali

Friday, October 24, 2014

UMOJA WA AFRIKA (AU) WAWATUNUKU DKT. SALIM NA BALOZI MBITA TUZO 


Waziri Mkuu Mstaafu, Dkt. Salim Ahmed Salim akipokea Tuzo ya Juu ya Umoja wa Afrika ya Mwana wa Afrika kwa Mwaka 2014 kutoka kwa Kamishna wa Amani na Usalama wa Umoja wa Afrika, Mhe. Balozi Smail Chergui. Tuzo hiyo  ilitolewa mjini Arusha pembezoni mwa Warsha ya Tano ya Ngazi ya Juu kuhusu Amani na Usalama Bararani Afrika iliyoandaliwa na Umoja wa Afrika inayoendelea mjini humo.

Balozi Chergui akimkabidhi Cheti cha Tuzo hiyo Dkt. Salim

Balozi Chergui akimkabidhi Tuzo ya Juu  ya Umoja wa Afrika ya Mwana wa Afrika ya Mwaka 2014, Binti wa Balozi Hashim Mbita, Sheila Hashima Mbita ambaye aliipokea Tuzo hiyo kwa niaba ya Baba yake ambaye hakuweza kufika kutokana na matatizo ya kiafya.(P.T)

Balozi Chergui akimkabidhi Cheti Bi. Sheila Hashim Mbita kwa niaba ya Balozi Mbita.