TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Thursday, February 28, 2013

HATUNA MPANGO WA KUWASAIDIA WALIOFELI KIDATO CHA IV - MULUGO


Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo, amesema wizara haina mpango wowote kwa sasa kuhusiana na wanafunzi waliofeli kidato cha nne mpaka pale Tume itakapomaliza kufanya kazi yake ndipo itaamua nini cha kufanya.
 
Mulugo aliliambia NIPASHE kuwa wizara inasubiri Tume iliyoundwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, imalize kufanya kazi yake, ndipo itatoa uamuzi nini kifanyike juu ya wanafunzi hao.
 
“Kwa sasa siwezi nikasema chochote kwani tume imeundwa ili kulifanyia kazi jambo hilo, hivyo tunasubiri wamalize kufanya kazi yao ndipo tutatoa kauli ya nini kifanye juu ya wanafunzi walio feli kama ni kurudia tena mtihani au la,” alisema Mulugo.
 
Alitoa ufafanuzi huo baada ya kuulizwa wizara yake inazungumziaje juu ya mpango wa Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Iringa, Jesca Msambatavangu kuandaa mafunzo ya kozi ya muda mfupi kwa vijana wote waliofeli mkoani humo ili kuwapima kama wapo wanaaoweza kusaidiwa kuendelea na elimu ya cheti.
 
Msambatavangu alitoa uamuzi huo baada ya makubaliano yake na baadhi ya vyuo vikuu kama Chuo Kikuu cha Tumaini (IUCO) na Chuo kikuu cha Ruaha (Ruco) na kukubaliana kutoa mafunzo hayo yatakayo anza Machi mwaka huu. 
 
Mulogo alisema kuwa ni wazo lenye mpango mzuri wa kuwasaidia vijana wengi ambao ni kama wamekumbwa na tatizo kwa sasa, hivyo anacho kifanya Mwenyekiti huyo hakina madhara yoyote  na anafanya kama raia mwema aliyeguswa na matokeo hayo
CHANZO: NIPASHE

HIZI NDO SABABU ZILIZOMFANYA PREZZO ASHINDWE KUHUDHURIA MAZISHI YA MPENZI WAKE, GOLDIE


Prezzo anaonekana akiwa amevaa nguo nyeusi zote, hii ilikua ni ibada ya kumuombea Goldie ambayo ilifanyika siku kadhaa kabla ya Prezzo kuondoka Nigeria kurudi Kenya.

 Ni watu wengi wanajiuliza imekuaje CMB Prezzo hajaonekana kwenye msiba wa mpenzi wake ambae walikua na plans za kuoana, Mnigeria Goldie aliefariki muda mfupi tu baada ya kufika Nigeria akitokea Marekani.
 
Kwa sababu nimeamua kumuacha Prezzo apumzike kwa sasa, ili kujua angalau hata kwa muhtasari niliamua kumtafuta Arthur Samwel ambae ni Dj wake na msimamizi wa kazi nyingi anazofanya Prezzo.
Andrew Harvey akimuaga mke wake Goldie siku ya maziko.
 
Najua siku chache kabla ya Goldie kuzikwa, vyombo vya habari kadhaa vya Nigeria viliandika kwamba mume wa Goldie, Andrew Harvey ambae ni raia wa Uingereza alimtumia ujumbe Prezzo akiwa Nigeria kwamba alichofanya basi inatosha, hatotaka kumuona tena akiwa karibu na familia ya Goldie.

Alichosema Arthur kuhusu Prezzo kutomzika Goldie ni hiki “Prezzo alirudi Nairobi wiki iliyopita, ilikua ni weekend na mpaka anatoka Lagos alikua hajui ni siku gani Goldie atazikwa kwa sababu Wanigeria wanatabia ya kuchelewa kuzika, sasa mtu kama uko ugenini huwezi kukaa muda wote…….. 
 
kwa bahati mbaya Prezzo akiwa amesharudi Nairobi alipigiwa simu kwamba Goldie ameshazikwa hivyo ikawa ni ngumu kurudi tena Lagos, sasa hivi yuko Eldoret Kenya kwenye ishu za kampeni”

LINEX AMVISHA PETE MCHUMBA WAKE AMBAYE NI MZUNGU

Mambo ya madini  

Wapendanoooooooo safi sana

Full kuringishia madini!!
Weekend hii, mtu mzima Sunday Mjeda aka Linex aka Mr VOA (Voice Of Africa),alifanya yake kwa kumvisha pete mpenzi wake, ambae ni  ambae ni  mwenyeji wa Finland anaeitwa Suvi.

 According to sources Linex aliamua kufanya kimya kimya tena wakiwa wawili tu, kwasababu hakutaka kujionyesha, na anaamini ile ni kitu  very personal haikuhitaji manjonjo mengi.

Well hongera zao na tunawatakia kila la kheri.
BOSI TAZARA AFURUMUSHWA KAZI
article_thumbs.php
Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA) Bw. Akashambatwa Mbikusita-Lewanika, hatimaye ameachia ngazi baada ya kuendesha kampeni kali ya miezi kadhaa kutaka aendelee kuongoza Mamlaka hiyo kwa miaka mingine mitatu.
 Hatua hiyo ya kuachia ngazi imekuja baada ya Bodi ya Wakurugenzi na Baraza la Mawaziri la Mamlaka hiyo kuonyesha dhahiri kutotaka Mzambia huyo aendelee na uongozi wa TAZARA kutokana na utendaji wake mbovu na uongozi mbaya uliowabagua wafanyakazi wa Mamlaka hiyo kwa misingi ya utaifa wao.
Habari za ndani za Mamlaka hiyo zimesema Bw. Akashambatwa ambaye kipindi chake cha uongozi kiliisha tarehe 22 Januari, 2013 kiliongezwa kwa maombi maalum ya Serikali ya Zambia kwamba Serikali hiyo ilihitaji muda mrefu kidogo kumpata mbadala wake, licha ya Serikali ya  Tanzania kutoridhishwa na utendaji wake.
Katika kikao chake cha tarehe 20 Februari, 2013 jijini Lusaka, Zambia, Baraza la Mawaziri lilijadili kwa siri na kwa kirefu suala la mtendaji Mkuu huyo ambaye inasemekana aliombewa tena na Serikali ya Zambia kipindi cha nyongeza, ombi ambalo inadaiwa lilipingwa vikali na ujumbe wa Serikali ya Tanzania ukiongozwa na Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe.
Taarifa za uhakika ndani ya Wizara ya Uchukuzi zinasema Serikali ya Tanzania haikumtaka Mtendaji Mkuu huyo kwa sababu kadhaa zikiwemo :uwezo mdogo, ubadhirifu, kuchochea ubaguzi kati ya Watanzania na Wazambia, ukaidi na uchochezi. Inadaiwa kuwa Mtendaji Mkuu huyo alizuia kuanzishwa kwa mradi wa usafiri jijini Dar es Salaam bila sababu yoyote ya msngi na kuishia kusambaza taarifa za uongo na uchochezi Zambia na magazeti mbalimbali nchini.
Tarehe 25 Februari, 2013 Gazeti la kila siku la Zambia, Zambia Daily Mail, liliripoti tukio hilo la kuachia ngazi kwa kiongozi huyo ambaye anajulikana sana nchini Zambia kama mfanyabiashara na kiongozi wa kimila (chief),                                             
Gazeti hilo lilinukuu barua ya Bw. Akashambatwa ya tarehe  22 Februari, 2013 kwenda kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Ujenzi, Ugavi na Mawasiliano ya Zambia, akielezea kuwa hakuna faida ya kuomba kurefushwa kwa mkataba wake wakati vyombo vikuu vya uongozi vya TAZARA, Bodi ya Wakurugenzi na Baraza la Mawaziri, havionyeshi kumkubali.
Kuondoka kwa Bw. Akashambatwa kwenye uongozi wa TAZARA kunatarajiwa kupokewa na wafanyakazi wa TAZARA kwa nderemo na vifijo.

MWANA FA ADAI KUWA SIRI YA MAFANIKIO YAKE NI MATUMIZI MAZURI YA VIPAJI ALIVYO NAVYO

MSANII wa muziki wa kizazi kipya Hamis Mwinjuma 'Mwana Fa' aeleza, kuwa na kipaji zaidi ya kimoja ndio sababu ya kipekee inayomtofautisha yeye pamoja na kazi zake na baadhi ya wasanii wengine wa muziki wa bongofleva
 
Aliyazungumza hayo jijini Dar es Salaam wakati akielezea mikakati yake aliyokuwa nayo ya kuiachia nyimbo yake mpya hivi karibuni inayoitwa 'Kama Zamani'ambapo mashabiki wake watapata fursa ya kuisikia nyimbo hiyo katika vituo vya redio mbalimbali nchini, alisema kipaji ndicho kinachompa fursa ya kufanya muziki katika ngazi ya kimataifa

Alisema muziki unamatawi mbalimbali kwani kuna baadhi ya wasanii wanakipaji cha kuimba tu lakini hawezi kufanya shoo katika 'stage' wapo baadhi wanajua kuandika na hawajui kuimba wapo wengine wanajua kufanya vyote kwa wakati mmoja

Akizungumzia kwa upande wake Mwana Fa alisema amejaaliwa kuwa na vipaji vyote kwa wakati mmoja huku akiwa na uwezo wa kuandika mashairi, kuimba pamoja na kulimiliki jukwaa pindi awapo katika shoo

"Nimejaliwa vipaji vyote hivyo, kwani nina uwezo wa kuandika mistari mizuri, kuimba na kulimiliki jukwaa na ndio maana shoo zangu zinakuwa na mvuto wa kipekee kutokana, sanaa na ubunifu niliokuwa nao " alisema Mwana Fa

Akizungumzia ujio wa wimbo wa 'Kama zamani' wenye mahadhi ya Hip Hop ambapo msanii huyo amewashirikisha baadhi ya wasanii kama Man'dojo, Domokaya na The Kilimanjaro Band (Wana Njenje), alisema kuwa ameamua kushirikisha wasanii hao ili kuleta radha tofauti ya muziki na mashabiki wapate muziki ulio bora

Alisema kuwa nyimbo hiyo italeta mabadiliko makubwa katika tasnia ya muziki kulingana na ubora uliopo, kwani imetengenezwa 'live' kinanda, gitaa vyote vinasikika kwenye muziki huo, chini ya mtayarishaji Pfunk Majani

PAPA AWAAGA RASMI WAUMINI WA KANISA CATHOLIC

-UTUMISHI wake unakoma rasmi leo, aaga kwa mawingu mazito, jua lawaka ghafla
 
ILE historia ambayo haijawahi kuwepo kwa miaka 600 iliyopita ya papa kujiuzulu inafikia tamati leo Alhamisi ambapo Papa Benedict XVI anaachia rasmi uongozi wa Kanisa Katoliki Duniani.

Jumapili iliyopita katika Uwanja wa Kanisa la Mtakatifu Petro, jijini Vatican, maelfu ya waumini wa madhehebu hayo walijitokeza kumuaga wakati alipowabariki katika ibada yake ya mwisho wa utumishi ambapo alisema itakuwa leo Februari 28, 2013.

Papa mwenye umri wa miaka 85 ambaye ni mzaliwa wa nchini Ujerumani aliwaambia waumini hao waliokadiriwa kufikia laki moja (100,000) kuwa, Mwenyezi Mungu amemuita kwa njia nyingine na kwamba kujiuzulu kwake ni matakwa yake binafsi wala hakuna shinikizo.

Papa aliyasema hayo kwa sauti yenye nguvu na mamlaka lakini iliyokuwa ikiashiria kutetemeka ambapo umati huo ulijikuta ukijawa na simanzi.

 
Awali mawingu mazito yalitanda na mvua kubwa kutarajiwa kunyesha jijini humo na watu kuhofia kujitokeza, lakini kengele ilipolia kuashiria muda wa papa kuzungumza na watu umewadia, mawingu yalitoweka na kuacha jua likimulika kwenye anga ya bluu jambo ambalo papa huyo alimshukuru Mungu kwa kusema:

“Tunamshukuru Mungu kwa kutupatia jua,” kauli iliyoibua furaha kwa watu.


Jijini Dar es Salaam habari za uhakika zinasema kuwa, Kadinali Pengo aliondoka wiki iliyopita kwenda Vatican kuhudhuria zoezi la mchakato wa kumchagua papa mpya.

"SINA UHUSIANO WOWOTE NA MASTER J...MPENZI WANGU ATATAMBULIKA BAADA YA KUFAHAMIKA KWA WAZAZI"...SHAA

Shaa na Master J.
Hii interview ya Shaa kwenye Leo Tena ya Super Brand Clouds FM......

Ni kuhusu alichosema kuhusu taarifa za uhusiano wake na Producer Legend Tanzania Master J, ilikua ni interview ambayo hata mimi nilienjoy kuisikiliza manake Dina Marios na Shaa na wengine waliokuwepo studio walikua wamechangamka sana alafu Shaa alijiachia vizuri pia.
 
Alichojibu Shaa kwenye maswali ya ndio au hapana ni hapana, akisema “Ndugu mtangazaji hapana, hatuna uhusiano wowote”

Kwenye mstari mwingine Shaa alisema mpenzi wake atatambulika baada ya wazazi wake kumfahamu na kupokea mahari, baada ya hapo sasa kadi za mwaliko ndio zitaweka ukweli ambao wengi wanataka kuujua.

Basi baada ya kusoma hii stori ya Shaa natumia nafasi hii kukualika kuisikiliza hii hit song ya Promice ambayo iliandikwa na Barnaba Boy, support cha home.

RICK ROSS AONGEZEWA ULINZI ZAIDI BAADA YA KUANDAMWA NA WAHUNI......

Rick Ross, rapper ambaye amekuwa akilengwa kushambuliwa na kundi la wahuni, ameongezewa ulinzi na polisi wa jijini New York, Marekani…. saa 24 kwasababu ya kupokea vitisho vingine.
Rick+Ross+Backstage+BET+Rip+Runway+Show+m6WNbNdVxn7l
Kwa mujibu wa mtandao wa TMZ, polisi wamekuwa wakimlinda Ross aliyefikia kwenye hoteli ya The London kwa siku za hivi karibuni. Vyanzo vimeuambia mtandao huo kuwa vitisho vipya dhidi ya rapper huyo mwenye makazi yake jijini Miami, Florida hajavichukulia kawaida.

Mwezi uliopita Ross akiwa anaendesha gari lake aina ya Rolls-Royce alinusurika kupigwa risasi huko Ft. Lauderdale muda mfupi baada ya kutoka kwenye party ya kusherehekea siku yake ya kuzaliwa. Hata hivyo yeye na msichana aliyekuwa naye hawakujeruhiwa.
NIKKI MBISHI AMMWAGIA SIFA KIBAO LADY JAY DEE

Nikki Mbishi ni rapper usiyeweza kumfananisha na yeyote Tanzania kwa uwezo wake usioelezeka katika uandishi wa haraka wa mashairi yenye mistari konde na uwezo wa kufanya mitindo huru (freestyle). Pia ana kumbumbuku ya ajabu na akiwa na uwezo wa kuimba nyimbo za wakongwe kama Profesa Jay na hata wa Marekani utadhani kaziandika yeye.
mbishi na jide
 
 Lakini pamoja na maisha yake ya muziki kuzungukwa zaidi na utamaduni wa Hip Hop, Nikki aka Terabyte huchukua muda pia kusikiliza muziki laini wa wasanii wenzake wa Bongo na kwa mtazamo wake Lady Jaydee ndiye msanii wa kike anayemkubali kuliko yeyote.

“Leo nimeamka na dada mkuu tu @JideJaydee hakuna kama huyu kwenye historia ya wanamuziki wa kike Bongo @GraceMatata fuata huyo dada.,” ametweet Nikki Mbishi.

Rapper huyo controversial ameendelea kutweet majina ya nyimbo kibao za nguli huyo wa muziki wa Tanzania ambaye jina lake halisi ni Judith Mbibo.

MGAO WA UMEME WAMKERA SALAMA JABIR....

Siku za hivi karibuni kumekuwepo na katizo la umeme la mara kwa mara katika maeneo mengi ya jiji la Dar es Salaam kiasi cha kuathiri shughuli nyingi za kiuchumi.
484946_146643805496139_968742939_n
Kufuatia tabia hiyo ya Tanesco kufanya yao kila siku na kuwaweka wajasiriamali wanaotegemea umeme kwenye mawe, mtangazaji wa kipindi ca Mkasi, Salama Jabir, ameamua kuzipunguza hasira zake kwenye Twitter kwa kuandika:

Kazi inabidi ziende jamani…The f**k is wrong na hii nchi?!Umeme tu?????!Shida isotatulika miaka nenda rudi?!Tunachoshaaaana. F**k that shit!! Taarifa hakuna…kuunguziana mali tu,kulipa hamlipi,kauli nzuri hamna!! Who does that?! Well..Mnatufunza sana,Asanteni!!

Watu wakiamua kuishi nje serikali inalalamika Ooh vijana hawana upendo na nchi yao!!Utapendaje nchi inayokurudisha nyuma? What the f**k?! Well KZMZ!!! 

Alosema bora mthamini mbwa naona hakuwa mbali na Ukweli..Ki ukweli misemo ya wahenga yote ni ukweli mtupu, again…KZMZ.

Nimejipigapiga mwenyewe nikanunua kaTV ka kitundika ukutani kama tunazoziona kwenye TV mkaunguza,nikarudisha dukani watengeneze.
MSD KWENYE MAONESHO YA HUDUMA ZA TIBA
00ab1 8104f
Ofisa Huduma kwa Wateja wa Bohari ya Dawa (MSD),Florida Sianga (kulia)) akiwaelekeza Monica Gofrey (kushoto) na Geofrey Kandi kifaa tiba aina ya sterilizer inayotumia gesi katika maonesho ya Shirikisho la Wadau wa Huduma za Afya Kusini Mwa Afrika, jana kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam. (PICHA NA KAMANDA WA MATUKIO BLOG

00ab 5df94
MNYIKA ALIA NA MGAO WA UMEME

Mbunge wa jimbo la Ubungo-Chadema Mh John Mnyika-

Nchi imeingia tena katika mgawo wa umeme kinyume na ahadi iliyotolewa na Waziri wa Nishati na Madini Prof Sospeter Muhongo bungeni tarehe 28 Julai 2012. Hali hiyo ni matokeo ya Serikali kutozingatia tahadhari niliyoitoa bungeni tarehe 27 Julai 2012 kwa niaba ya Kambi Rasmi ya Upinzani na kwa nyakati mbalimbali kwa nafasi yangu ya Waziri Kivuli wa Nishati na Madini juu ya hali tete iliyotarajiwa kuwepo na hatua zinazopaswa kuchukuliwa katika utekelezaji wa mpango wa dharura wa umeme.

Ikiwa ni sehemu ya wajibu wa kibunge wa kuisimamia Serikali nawataka viongozi na watendaji wa Wizara ya Nishati na Madini na Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) kuacha kuficha hali ya mambo na kuwaeleza ukweli wananchi kuhusu mgawo wa umeme uliojitokeza na hatua za haraka zinazochukuliwa kurekebisha hali hiyo. 
 Iwapo Wizara na TANESCO hawatatoa matangazo ya ukweli kwa wananchi, kwa nafasi yangu ya Waziri Kivuli wa Nishati na Madini nitaeleza vyanzo vya mgawo wa umeme uliojitokeza ili hatua ziweze kuchukuliwa wakati huu ambapo wajumbe wa kamati ya nishati na madini wenye wajibu wa kuisimamia Serikali kwa niaba ya Bunge katika sekta hizo nyeti hawajateuliwa.

 Aidha, pamoja na kutoa maelezo kuhusu mgawo wa umeme, Wizara ya Nishati na Madini na TANESCO watumie nafasi hiyo pia kueleza hatua zilizochukuliwa kuhusu ukaguzi wa awamu ya pili kuhusu tuhuma za ufisadi katika ununuzi wa vifaa na uzalishaji wa umeme wa dharura ikiwemo kuhusu mafuta mazito ya kuendeshea mitambo ya kufua umeme. 
Ikumbukwe kwamba mwanzoni mwezi Agosti 2012 Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (NAOT) iliunda timu ya wakaguzi kufanya ukaguzi maalum wa hesabu za Shirika la Umeme (TANESCO) kufuatia tuhuma za ubadhirifu wa fedha za umma zilitajwa bungeni na Waziri Kivuli wa Nishati na Madini katika maoni ya Kambi Rasmi ya Upinzani tarehe 27 Julai 2012 na Waziri wa Nishati na Madini wakati wa majumuisho ya hoja ya Serikali tarehe 28 Julai 2012. 
 Wizara ya Nishati na Madini na TANESCO waeleze pia hatua iliyofikiwa kuhusu uchunguzi mwingine uliofanywa na Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) kuanzia mwezi Agosti 2012 wa mchakato wa ununuzi wa mafuta mazito ya kuendeshea mitambo ya kufua umeme wa dharura kutokana na tuhuma mbalimbali zilizotolewa bungeni kuhusu ununuzi huo suala ambalo Kambi Rasmi ya Upinzani ilitaka pia tarehe 27 Julai 2012 liundiwe kamati teule ya Bunge ili uchunguzi wa kina uweze kufanyika. 

 Wenu katika uwakilishi wa wananchi, 

John Mnyika (Mb)
Waziri Kivuli wa Nishati na Madini 

27 Februari 2013

Wednesday, February 27, 2013

MSANII OMOTOLA ANG'AA HOLLYWOOD

Muigizaji wa Nollywood, Omotola, Jalade- Ekeinde, ameanza kuonekan kwenye televisheni za Marekani, kwenye kipindi kiitwacho Bounce

Nyota huyo ambaye amekuwa Marekani kwa muda sasa ameanza kuonyesha uwezo wake mbele ya wakali wa Hollwood nchini Marekani

Baadhi ya wasanii mbalimbali kutoka Nigeria walishindwa kung'aa lakini msanii huyo amefanikiwa kushiriki kwenye tamthilia nchini Marekani

Katika tamthilia hiyo Omotola amecheza na Kimberly Elise

VIDEO ZA MZIKI WA MTOTO WA MIAKA 9 ZALETA BALAAA


Mtoto mwenye umri wa miaka 9, Luie Rivera Jr., ambaye jina lake la kisanii ni “Lil Poopy,” ameonekana kwenye video anazozipost online hususan kwenye mtandao wa YouTube, akicheza muziki na wasichana wakubwa kwa umri wake, akiendesha magari ya kifahari kama Ferrari na akirap maneno kama “coke is not a bad word.” 

Katika video nyingine mtoto huyo anaonekana akicheza na msichana katika pozi chafu huku watu wakimtupia hela.
poopyladies
Idara ya polisi ya Brockton, Massachusetts, imewasiliana na ofisi inayoshughulikia masuala ya watoto na familia nchini humo baada ya kupokea simu nyingi kutoka kwa watu walioguswa kufuatia kuona video zake.
lil-poopy-584x350
Baba wa rapper huyo Luie Rivera ameajiri mwanasheria kujilinda na uwezakano wa kukamatwa kwa kosa la jinai.

SERIKALI YA UGANDA YAJIPANGA KUWANUNULIA WABUNGE WAKE TOLEO IPYA LA IPAD ILI KUPUNGUZA GHARAMA ZA STESHENARI


Chama cha Forum for Democratic Change (FDC) kimepokea na kukubali mpango wa serikali ya Uganda wa kununua toleo jipya kabisa la iPads kwa ajili ya wabunge, lakini kimesema wabunge hao wakopeshwe na sio wapewe bure.
 
Msemaji wa Chama hicho Wafula Oguttu ambae pia ni mbunge, amesema pendekezo la kununua iPads halikataliwi lakini hakuna sababu ya kuwapa bure na badala yake wapewe kwa mkopo.
 
Serikali ya Uganda imepanga kununua iPads za kisasa na kuwapatia wabunge kwa lengo la kupunguza gharama ya steshenari.
 
Uamuzi huo ulichukuliwa hivi karibuni na Kamati ya Bunge na unasubiri utekelezaji kwa Kamati ya Mikataba.
RAY: MAZOEZI YAMENISAIDIA KUPUNGUA
Picha hiyo ya juu inamuonesha alivyokuwa mwanzo (kushoto) na jinsi alivyo sasa (kulia).
------------
Muigizaji aliyepo kwenye list A ya waigizaji wa filamu Tanzania, Vincent Kigosi aka Ray ameamua kuzungumza baada ya watu kuanza kumzushia anaumwa kutokana na kupungua mwili wake kwa kiasi kikubwa.

Ray amezikanusha tetesi hizo zilizoanza kusambaa kwa haraka ambapo gazeti la udaku la Kiu wiki hii lilikuwa na habari isemayo, ‘Ray apukutika mwili’ – Kitambi chote kwishnei! Ukimuona unaweza kumpita bila kumtambua, maombi ya wakatoliki yahusishwa.

Hata hivyo Ray amesema hali hiyo imetokana na kufanya mazoezi zaidi siku za hivi karibuni. “Jamani kwani unene ndio afya au kupungua ndio ugonjwa,” ameuliza Ray.
CHOCOLATE ZAMPONZA WEMA SEPETU 

CEO wa Endless Fame Films Wema Sepetu amelazimika kujisamilisha kwa daktari wa meno baada ya ulaji wa chocolate kumponza na hivyo kuozesha baadhi ya meno yake.
eb53b55080ba11e2bd6422000a9f12df_7
Kupitia Instagram, Miss Tanzania huyo wa zamani, ameshare picha akiwa kwenye clinic ya meno kung’oa jino lililokuwa likimsumbua. “Apparently I have 8 cavities…. oh god… does this mean no more chocolate for me,” ameandika. Kwa waliowahi kuumwa na jino wanaujua muziki wake, so get well soon Wema.
JK ATEMBELEA JKT
jkt1
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na uongozi wa juu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) jijini Dar es salaam alipotembelea leo February 27, 2013. Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Vuai Shamsi Nahodha, Mkuu wa Majeshi Jenerali Davies Mwamunyange pia walihudhuria.

jkt5
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na uongozi wa juu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) jijini Dar es salaam alipotembelea leo February 27, 2013. Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Vuai Shamsi Nahodha, Mkuu wa Majeshi Jenerali Davies Mwamunyange pia wapo.
jkt6-
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akielekea kwenye uwanja wa sherehe baada ya kupata maelezo na kutoa maagizo kwa  uongozi wa juu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) alipotembelea makao makuu yake  leo February 27, 2013. Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Vuai Shamsi Nahodha na Mkuu wa Majeshi Jenerali Davies Mwamunyange pia walihudhuria.
jkt7-
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipokea zawadi ya saa toka kwa  Mkuu  wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Meja Jenerali Raphael Muhuga huku  Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Vuai Shamsi Nahodha, Mkuu wa Majeshi Jenerali Davies Mwamunyange wakishuhudia. Saa hiyo imeandaliwa na makamanda wa JKT kumpongeza Rais Kikwete kwa kurejesha mafunzo ya jeshi la ulinzi kwa mujibu wa sheria kuanzia mwaka huu.

jkt9-
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia makamanda wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) alipotembelea makao makuu yao leo February 27, 2013
jkt14-
PINDA AZINDUA GSI TANZANIA
IMG_0056
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akikata utepe kuashiria uzinduzi  wa Mpango  Mkakati  wa Miaka Mitano  wa Taasisi  ya  GSI Tanzania  kwenye ukumbi wa hoteli ya Blue Pearl  jijini Dar es salaam Februari 27, 2013. Wa pili kulia ni Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko, Dr.Abdallha Kigoda. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Joyce Mapunjo.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

IMG_0099
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akitazama mikoba katika maonyesho yaliyoambatana na Uzinduzi wa  Mpandgo Mkakati wa Miaka  Mitano wa Taasisi  ya GSI Tanzania kwenye ukumbi wa Hoteli ya Blue Pearl jijini Dar es slaam Februari  27, 2013. Kushoto ni Waziri wa Viwanda,Biashara na Masoko, Abdallah Kigoda na kulia ni  Katibu  Mkuu wa Wizara hiyo, Joyce Mapunjo. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
PAPA WAWILI KATIKA MGONGANO



Na  VATICAN City, Vatican 
 YAMETIMIA. Safari ya miaka saba ya Baba Mtakatifu Benedict XVI inakamilika leo pale atakapong’atuka rasmi katika uongozi wa Kanisa Katoliki, ifikapo saa 2:00 usiku kwa saa za Italia (saa 4:00 usiku kwa saa za Tanzania).
Kwa siku mbili, Papa amekuwa na shughuli nyingi katika makao yake, Gandolfo Castel, Vatican akijiandaa kimwili kuondoka, akiweka sawa nyaraka zake binafsi na zile za kanisa ambazo zitawekwa katika kumbukumbu.
 Kwa upande mwingine Vatican, nchi ambayo ipo ndani ya Jiji la Rome iliyozungukwa na ukuta, ikiwa na ukubwa wa hekta 44 na wakazi 832 pekee, imekuwa katika hekaheka nyingi.
Jana, waumini zaidi ya 50,000 na wengine wengi kutoka sehemu mbalimbali duniani wakiwamo makardinali, maaskofu, mapadri na walei walialikwa kwa shughuli rasmi ya kumuaga kiongozi huyo.
Tofauti na kanuni yake, leo Benedict hatavaa viatu vyekundu kama ilivyozoeleka na badala yake amechagua viatu rahisi vya ngozi vilivyobuniwa Mexico. Alipewa viatu hivyo ikiwa ni zawadi wakati wa ziara nchini humo 2012.
Tangu alipotangaza uamuzi wake wa kung’atuka Februari 11, mwaka huu, utata umegubika nafasi yake katika maisha mapya ndani ya Vatican, akiitwa Papa Mstaafu.
Waumini, wataalamu na hata viongozi mbalimbali wa Kikatoliki wameanza kuhoji ni jinsi gani viongozi wawili (Papa) wataishi, huku wote wakivaa mavazi meupe wakiitwa Papa, wakiishi umbali mdogo kati yao, wakiwa na wasaidizi wengi wanaowahudumia.
Vatican
Nje ya Gandolfo Castel, ulinzi umeimarishwa na vibali vya kuingia Vatican vimesitishwa.
Juzi, Vatican ilitangaza kwamba Papa Benedict XVI atajulikana kama ‘Emeritus Pope’, yaani Papa Mstaafu mwenye cheo cha heshima, akiendelea kuitwa, ‘mtakatifu’ na ambaye ataendelea kuvaa nguo nyeupe.
Mavazi na hata jina lake jipya ni masuala ambayo yamezua uvumi mwingi, huku suala la mrithi wake mpya pia likiwa gumzo, kwani tukio kama hilo lilitokea miaka 600 iliyopita.
Ni uamuzi uliolishtua kanisa hilo lenye waumini 1.2 bilioni duniani na wengi wanasema awali, haikushauriwa Papa kustaafu kwani kwa kufanya hivyo kunaacha mizozo na minong’ono ya kuwania madaraka.
Hata hivyo, uongozi wa Vatican umesisitiza kuwa uamuzi huo wa Papa Benedict XVI ni wa kipekee na hakuna mzozo ambao utatokea baina yake na mrithi wake ambaye mchakato wa kumpata unatarajiwa kuanza ndani ya wiki mbili zijazo.
“Kulingana na mabadiliko katika kanisa letu, kuna Papa mmoja. Ni dhahiri kwamba katika hali ya sasa hakutakuwa na tatizo,” anasema Mhariri wa Gazeti la L’Oservatore Romano linalomilikiwa na Vatican, Giovanni Maria Vian.
Hofu iliyopo
Hata hivyo, wakosoaji wa mambo hawakubaliani na hoja hiyo na baadhi ya makardinali walioko Vatican kwa usiri mwingi, wanazungumzia suala hilo wakieleza kwamba litazua tatizo kubwa kwa Papa ajaye, hasa ikiwa mtangulizi wake, Benedict akiwa bado hai.
Mtaalamu wa tauhidi (theolojia), raia wa Uswisi, Hans Kueng ambaye amekuwa mtu wa karibu wa Papa Benedict XVI, ingawa kwa sasa ni mkosoaji wake amesema:
“Kwa sasa, Benedict XVI akiwa bado hai, kuna hatari ya kuwa na Papa kivuli, mwenye mamlaka kamili ambaye kwa chinichini anaweza kumshinikiza mrithi wake kufikia uamuzi.”
Hans Kueng alisema hayo alipozungumza na Gazeti la Der Spiegel la Ujerumani.
Msemaji wa Vatican, Padri Federico Lombardi alisema Papa Benedict XVI kwa upande wake aliamua aitwe Papa Mstaafu au ‘kiongozi mstaafu wa Roma.’ Anasema haelewi ni kwa nini ameamua kuacha jina lake la sasa la Askofu wa Rome.
Kwa wiki mbili zilizopita, maofisa mbalimbali wa Vatican wamekuwa wakifikiri kwamba Papa angeanza kuvaa mavazi meusi na kutumia jina la Askofu Mstaafu wa Rome ili kuepuka mkanganyiko na mrithi wake.
Mwingine ambaye amekuwa akizusha mkanganyiko ni Katibu wa Papa, Askofu Mkuu, George Gaenswein ambaye ataendelea kuwatumikia Papa wote wawili, yaani Benedict XVI kwenye Monasteri ndani ya Vatican na kazi yake ya kawaida ya kuwa kiranja katika nyumba ya Papa mpya.
Kwa upande wake, Papa Benedict XVI anasema anastaafu na sasa ataishi maisha ya sala na tafakuri ya kina, mbali na majukumu mengine ya kidunia.
Hata hivyo, bado atakuwapo kwenye nchi ndogo ya Vatican, mahali ambako makazi yake yatakuwa jirani na mnara wa kurushia matangazo wa Kituo cha Redio cha Vatican, akiliangalia vizuri Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro.
Kwa upande wake, Kueng anasema ni kosa kwa Askofu Gaenswein kuwatumikia Papa wawili kwa wakati mmoja na pia Benedict XVI kubakia jirani na mahali hapo.
“Hakuna padri ambaye anapenda mtangulizi wake kuishi karibu naye na kufuatilia anayoyafanya.
Hata kama Askofu wa Rome, haipendezi kutenda kazi huku mtangulizi wako akiona na kufuatilia.”
Mbali na mitazamo hiyo, wengine wamedhani kuwa uamuzi wa Papa Benedict XVI unalenga kudumisha utamaduni wa watangulizi wake.
“Ninashangazwa kuona Papa Benedict XVI akiendelea kuitwa mbarikiwa na kuvaa nguo nyeupe,” anasema Padri James Martin, Mtawa wa Jesuit pia mwandishi na mhariri, lakini baadaye anajirudi na kusema:
“Lakini sioni ajabu, mbona marais wastaafu wa Marekani, bado wanaitwa Rais? ni alama ya heshima kwake.”
Katika mkanganyiko huo, wapo wanaoamini kwamba yanayotokea yanatokana na nguvu ya roho mtakatifu, huku wengine wakipiga upatu kwamba ni zamu ya Afrika kutoa Papa na wanatajwa Makardinali Peter Turkson wa Ghana na Francis Arinze wa Nigeria.

Tuesday, February 26, 2013

RONALDO KUENDELEZA USHINDI WA MAGOLI
Gooooooohhh.....!

BARCELONA, Hispania
 

Cristiano Ronaldo aliendeleza rekodi yake safi ya kufunga magoli kwenye Uwanja wa Nou Camp baada ya kutupia mabao mawili wakati Real Madrid ikiifunga Barcelona mabao 3-1 na kutinga fainali ya Kombe la Mfalme kwa ushindi wa jumla wa mabao 4-2 usiku huu (Februari 26, 2013).
Straika huyo wa kimataifa wa Ureno alitupia goli la kwanza kwa penati na baadaye akaongeza la pili muda mfupi baada ya mapumziko wakati Real walipoendelea kutumia vyema mashambulizi yao ya kustukiza.
Raphael Varane akafunga la tatu katika dakika ya 68 wakati Jordi Alba akaifungia Barcelona goli la kufutia machozi katika dakika za kuelekea mwishoni mwa mechi.
Real Madrid sasa watacheza fainali na mshindi wa mechi ya kesho (Februari 27, 2013) kati ya Sevilla na Atletico Madrid. Katika mechi yao ya kwanza, Atletico walishinda 2-1.
Ronaldo sasa amefunga katika mechi zote sita zilizopita kwenye Uwanja wa Nou Camp na pia akaibuka kidedea katika vita yake binafsi dhidi ya hasimu wake Lionel Messi, ambaye 'alifunikwa' katika muda mwingi wa mechi kama walivyokuwa nyota wenzake Xavi, Iniesta, Cesc Fabregas, Pedro, Sergio Busquets na hata David Villa aliyeingia akitokea benchi katika kipindi cha pili.
Messi ambaye ni nahodha wa timu ya taifa ya Argentina, atakuwa na nafasi nyingine hata hivyo ya kujibu mapigo ya Ronaldo wakati watakakutana tena Jumamosi katika mechi ya mzunguko wa pili wa La Liga, Ligi Kuu ya Hispania kwenye Uwanja wa Santiago Bernabeu.
Katika mechi ya 'Clasico' ya leo, hakukuwa na mabadiliko makubwa kwenye kikosi cha Barcelona huku Andres Iniesta akianzishwa katika safu ya mashambulizi badala ya David Villa na hivyo kutoa nafasi kwa Cesc Fabregas kucheza katika eneo la kiungo.
Jose Mourinho alimpanga Varane, ambaye alicheza vizuri sana katika mechi yao ya kwanza dhidi ya Barca badala ya Pepe, na alishirikiana na Sergio Ramos katika safu 'ngangari' ya ulinzi ya Real Madrid na pia hakukuwa na nafasi kwa Kaka 'aliyefufuka' kivingine baada ya Angel Di Maria kuanzishwa katika nafasi ya winga wa kulia.
Barca walianza kwa kasi huku Iniesta akipiga nje kutoka umbali wa yadi 20 na baadaye Messi akapiga shuti lililopita pembeni kidogo ya lango kwa mguu wake usiotisha wa kulia wakati alipokuwa umbali wa takriban yadi sita tu kutoka langoni mwa Real Madrid. Mashambulizi hayo yalifanyika ndani ya dakika mbili za mwanzo.
JK AKAGUA UKUMBI WA MIKUTANO WA KIMATAIFA 
8E9U3337
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akikagua ukumbi  mkubwa wa mikutano multi-purpose conference Hall uliopo mtaa wa Shaaban Robert jijini Dar es Salaam.Ukumbi huo wa Serikali upo chini ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.Ujenzi wa Ukumbi huo uko katika hatua za mwisho na Rais Kikwete mbali na kuridhishwa na hatua hiyo ametoa maelekezo kwa wahandisi kutenga sehemu maalumu kwa Wapiga picha na waandishi wa habari ili waweze kufanya kazi zao kwa ufanisi.Rais Kikwete pia ameelekeza wahandisi kuweka viti na meza zinazohamishika ili kukidhi matakwa ya mikutano na vikao vya aina mbalimbali(picha na Freddy Maro)
 
8E9U3420
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akikagua ukumbi  mkubwa wa mikutano multi-purpose conference Hall uliopo mtaa wa Shaaban Robert jijini Dar es Salaam.Ukumbi huo wa Serikali upo chini ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.Ujenzi wa Ukumbi huo uko katika hatua za mwisho na Rais Kikwete mbali na kuridhishwa na hatua hiyo ametoa maelekezo kwa wahandisi kutenga sehemu maalumu kwa Wapiga picha na waandishi wa habari ili waweze kufanya kazi zao kwa ufanisi.Rais Kikwete pia ameelekeza wahandisi kuweka viti na meza zinazohamishika ili kukidhi matakwa ya mikutano na vikao vya aina mbalimbali(picha na Freddy Maro)
STORI KUHUSU RIHANA NA CHRIS BROWN KUFUNGA NDOA

Jarida maarufu (Star Magazine) limeripoti kwamba mastaa wa muziki Chris Brown na Rihanna wanampango wa kufunga ndoa mwishoni mwa July 2013 nyumbani kwa kina Rihanna huko Barbados.
Jarida hili limeendelea kutiririka kwamba kwenye ndoa hiyo wamepanga kusherehekea na watu mbalimbali wakiwemo wanaoamini kwamba Chris Brown amebadilika kitabia.
Ni harusi ambayo watu wote walioalikwa watakua wamesimama na wahudumu watakuepo kumfata kila mtu alipo, pia wale wachoraji wa tattoo watakuepo pia.
NMB WAPATA TUZO YA SUPER BAND

Mkuu wa masoko na mawasiliano wa NMB Imani Kajula akipokea tuzo ya super brand kutoka kwa mkurugenzi wa super brand East Africa Jawad Jaffer. 

Afisa Mtendaji Mkuu wa NMB, Mark Wiessing akizungumza na Mkurugenzi Mkuu wa Clouds Media Group, Joseph Kussaga (Kulia) na Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa NMB Imani Kajula. 
Baadhi ya wafanyakazi wa Idara ya Masoko na Mawasiliano wa NMB wakiwa na tuzo ya super brand 2013-2014.

Tuzo ya Super Brand huwa inatolewa kwa kila kampuni ambayo jasho lake limeonekana, jitihada za ufanyaji kazi pamoja na kutimiza vizuri hata wakati mwingine kuvuka mipaka kwa yaliyoahidiwa.
Sasa baada ya miaka saba ya uwekezaji endelevu katika kuboresha huduma, masoko na mtandao wa matawi, benki ya NMB yenye zaidi ya matawi 148, ATM zaidi ya 500, wateja wanaotumia NMB mobile zaidi ya 800,000 na huduma mbadala  kama internet banking, kituo cha huduma kwa wateja na POS imepewa heshima na zawadi ya tuzo hiyo mwaka huu.
Jingine ambalo ni moja ya sifa kubwa zilizoipa heshima NMB ni kwamba wateja wake sasa wanapata huduma popote walipo bila kuhitajika kwenda kwenye tawi la NMB, maboresho hayo yameiwezesha NMB kutunukiwa kuwa Super Brand mwaka 2013-2014.
KOCHA WA AZAM AFUNGIWA KWA KUVUA NGUO UWANJANI
Kocha Stewart Hall wa Azam akibebwa na wachezaji wake baada ya kutwaa Kombe la Mapinduzi visiwani Zanzibar.
Stewart Hall
Kocha wa Azam, Stewart John Hall amefungiwa mechi tatu na kupigwa faini ya Sh. 500,000 kwa kwa kosa la kushusha bukta yake huku akimlalamikia refa msaidizi wakati wa mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya timu yake na Kagera Sugar iliyochezwa Januari 26 kwenye Uwanja wa Azam Complex ulioko Chamazi jijini Dar es Salaam.

Adhabu hiyo imetolewa na Kamati ya Ligi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) iliyokutana mwishoni mwa wiki kupitia ripoti za michuano ya VPL na Ligi Daraja la Kwanza (FDL) msimu wa 2012/2013 inayoendelea hivi sasa na kufanya uamuzi mbalimbali.

Naye Kocha Msaidizi wa timu ya Mgambo Shooting, Denis Mwingira ametozwa faini ya sh. 500,000 kwa kumtolea lugha chafu mwamuzi kwenye mechi dhidi ya Mtibwa Sugar iliyochezwa Oktoba mwaka jana katika Uwanja wa Manungu.

Ally Jangalu ambaye ni Kocha Msaidizi wa Polisi Morogoro naye ameangukiwa na rungu la Kamati ya Ligi kwa kupigwa faini ya sh. 500,000 baada ya kutolewa kwenye benchi kwa kupinga uamuzi wa refa kwa sauti ya juu. Alitenda kosa hilo kwenye mechi kati yao na Kagera Sugar iliyochezwa Novemba 10 mwaka jana Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba.

Matukio ya aina hiyo kwa kocha Jangalu yamekuwa ya kujirudiarudia ambapo Oktoba 13 mwaka jana katika mechi dhidi ya Azam iliyochezwa mjini Morogoro aliondolewa na mwamuzi kwenye benchi kwa kuchochea wachezaji wa timu yake wacheze rafu.

Naye Kocha wa timu ya Moro United inayoshiriki FDL, Yusuf Macho amepigwa faini ya sh. 200,000 kwa kumtolea lugha chafu refa baada ya mechi dhidi ya Transit Camp iliyofanyika Novemba 4 mwaka jana Uwanja wa Mabatini mjini Mlandizi.

Pia Kocha wa Burkina Faso, Hasheem Mkingie amepigwa faini ya Sh. 200,000 baada ya kutolewa kwenye benchi kwa kutoa lugha chafu katika mechi ya FDL dhidi ya Mkamba Rangers.

Kiongozi wa Majimaji, Joseph Nswila ambaye aliingia uwanjani baada ya mechi dhidi ya Mlale JKT kumalizika na kuvamia waamuzi amefungiwa miezi sita.

Vilevile timu ya Azam imepigwa faini ya sh. 300,000 kwa kuchelewa kufika uwanjani kwenye mechi kati yao na JKT Oljoro iliyochezwa Novemba 7 mwaka jana katika Uwanja wao wa Azam Complex ulioko Chamazi, Dar es Salaam.

Pia Coastal Union imetozwa faini ya sh. 500,000 kutokana na washabiki wake kumrushia chupa za maji mwamuzi msaidizi namba mbili wakati wa mechi yao dhidi ya Simba iliyochezwa Oktoba mwaka jana Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga.

Nayo klabu ya African Lyon imepigwa faini ya sh. 500,000 kwa timu yake kugoma kuingia kwenye chumba cha kubadilishia nguo wakati wa mapumziko katika mechi dhidi ya Coastal Union iliyochezwa Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga, Oktoba 24 mwaka jana.

Timu ya Burkina Faso ya Morogoro imepigwa faini ya sh. 200,000 kutokana na kuonesha vitendo vya ushirikina kabla ya mechi yao dhidi ya Mbeya City iliyochezwa Oktoba 24 mwaka jana Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.

Faini ya ushirikina ya sh. 200,000 pia imepigwa timu ya Pamba baada ya kuonesha vitendo hivyo kwenye mechi yao dhidi ya Mwadui iliyochezwa Novemba 4 mwaka jana Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga.

Nayo Mkamba Rangers imepigwa faini ya sh. 200,000 baada ya washabiki wake kumtolea lugha chafu Katibu wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Morogoro (MRFA), Hamis Semka na kumrushia chupa za maji mwamuzi wa mezani katika mechi dhidi ya Mbeya City iliyochezwa mjini Morogoro.

Polisi Dodoma imepigwa faini ya sh. 200,000 kutokana na washabiki wake kuvamia uwanjani na kutaka kuwapiga waamuzi katika mechi yao dhidi ya JKT Kanembwa na kusababisha mipira miwili ya Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dodoma (DOREFA) kupotea.

Pia klabu kadhaa zimeandikiwa barua za onyo kwa timu zao kuchelewa kufika uwanjani au kutofika kwenye mkutano wa maandalizi ya mechi (Pre-match meeting). Klabu hizo ni Coastal Union, JKT Ruvu, Toto Africans, Simba, Green Warriors, Majimaji, Mkamba Rangers, Polisi Dodoma, JKT Kanembwa, Moro United.

Mchezaji Stanley Nkomola wa JKT Ruvu baada ya mechi dhidi ya Coastal Union alikwenda jukwaani na kuanza kupigana na washabiki. Pia kipa wa timu ya Transit Camp, Baltazar Makene baada ya mechi dhidi ya Tessema aliruka uzio na kwenda kupigana na washabiki.

Kwa vile masuala ya wachezaji hao ni ya kinidhamu yamepelekwa kwenye Kamati ya Nidhamu inayoongozwa na Kamishna wa Polisi (CP) mstaafu Alfred Tibaigana kwa ajili ya kuchukuliwa hatua.

TFF KUJADILI TAMKO LA SERIKALI
Sekretarieti ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imepokea barua ya Serikali ikielezea uamuzi wa Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mukangara kutengua uamuzi wa Msajili wa Klabu na Vyama vya Michezo nchini kuidhinisha marekebisho ya Katiba ya TFF toleo la 2012.

Baada ya kupokea barua hiyo jana alasiri (Februari 25 mwaka huu), Sekretarieti iliwasiliana na Rais wa TFF, Leodegar Tenga ambaye ameagiza kuitishwa kikao cha dharura cha Kamati ya Utendaji kujadili tamko hilo.

Kikao hicho cha Kamati ya Utendaji ya TFF kitafanyika Jumamosi (Machi 2 mwaka huu) jijini Dar es Salaam.
HUKUMU YA KAJALA YAPIGWA KALENDA

Hukumu iliyokuwa ikisubiliwa na baadhi ya wadau wa tasnia ya sanaa hususani upande wa filamu ya msanii wa bongo movi Kajala Masanja imehairishwa mpaka tarehe 25 mwezi wa tatu

Chanzo cha habari ambacho ni mmoja wa rafiki wake wa karibu na msanii huyo alieleza kuwa kutokana na kutokuwepo kwa baadhi ya wahusika katika kesi hiyo imemladhimu hakimu kuihairisha kesi hiyo mpaka tarehe iliyopangwa hapo juu
MCHUMBA WANGU ANANIPENDA ROSE NDAUKA ADAI
MSANII wa filamu nchini Rose Ndauka afunguka juu ya tatoo  alizochora mchumba wake Mariki Bandawe, zinazoonyesha mchoro wa kopa . Alisema kupitia mchoro huo ni dhahiri kuwa mchumba wake amedhihirisha kuwa na mapenzi ya dhati

Rose alilazimika kufunguka juu ya hilo baada ya kupokea maswali mengi kutoka kwa baadhi ya mashabiki wake kwenye mtandao wa kijamii 'Facebook' baada ya kuituma picha hiyo inayomuonyesha mchumba wake akiwa na mchoro kwenye bega lake la kushoto

Akizungumza na jarida la Maisha Rose alisema kuwa mchoro wa mchumba wake ni dhahiri kuwa ana mapenzi ya dhati kwani ni wanaume wachache wanaweza kufanya kitendo alichokifanya yeye na kutuma picha kama hiyo ambayo inaonekana na watu wengi
"Unajua mpaka mtu inafikia hatua ya kuweka wazi ni kwamba unajiamini na chaguo lako na pia kwa upande wangu inaonyesha kunijali na kunilinda na baadhi ya magonjwa maambukizi kwa kutojihusisha na mwanamke mwingine," alisem Rose

Pamoja na hayo alizungumzia juu ya harusi yake ambayo amesema kuwa muda ukifika ataweka wazi tarehe na mwezi wa siku yao ya kufunga ndoa

Picha hiyo ilionekana kuleta utata baada ya mchumba wake kuituma picha kwenye mitandao ya kijamii 'facebook' huku baadhi ya mashabiki wakituma maoni yao juu ya picha hiyo na kutaka kufahamu nini maana ya alama iliyokuwepo kwenye picha
NOKIA YAZINDUA SIMU INAYOTUNZA CHAJI KWA MWEZI MZIMA NA GHARAMA YAKE NI SH. 30,000 KWA MWEZI


Baada ya Nokia 1100 huenda Nokia 105 ikaja kuwa simu maarufu zaidi hasa kwenye nchi zinazoendelea ikiwemo Tanzania. Hii ni baada ya kampuni hiyo ya simu kuzindua simu hiyo yenye uwezo wa kutunza chaji kwa siku 35 kila unapochaji.
Simu hiyo imetengenezwa maalum katika maeneo ambayo umeme hakuna ama unasumbua lakini pia kama ‘backup phone’ pale zingine zinapozima.
nokia
Ikiwa inatarajia kuingia sokoni wiki kadhaa zijazo, Nokia 105 ambayo bei yake ni paundi 13, sawa na shilingi 30,000 za Tanzania pia ina tochi na FM radio.
LADY JAYDEE NA PROF JAY NDANI YA NGOMA MOJA 

Profesa Jay na Lady Jaydee wanapokutana siku zote huwa hapaharibiki kitu, ni hit tu. Baada ya miaka mingi kupita, nguli hao wamekutana tena na guess what, this time hakuna amani kabisa kati yao, ni Joto na Hasira tu.

Unakumbuka Profesa Jay ameshawahi kumshirikisha Jide kwenye nyimbo zake mbili zilizohit sana enzi zake, Bongo Dar es Salaam na Nimeamini? Lakini kumbukumbu zetu hazituambii kama tulishawahi kusikia wimbo ambao Lady Jaydee amemshirikisha Profesa Jay. Hivyo huenda huu ndio ukawa wa kwanza.

Kupitia Facebook jana Lady Jaydee aliandika:

Naomba ku share muonekano wa ndani wa CD ya wimbo wangu mpya “JOTO, HASIRA” feat Prof Jay ambao unatoka siku za karibuni.” Lady Jaydee aliwaomba mashabiki wake wamsaidie kuchagua kava la wimbo huo.