TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Wednesday, August 29, 2012

WATAALAM WA MAMBO YA AFYA KUTOKA NCHINI INDIA WAJA TANZANIA KWA ZIARA YA UTALII WA AFYA























Mshauri wa Ubalozi wa India Kunal Roy akiongea na Waandishi wa habari ambapo hawapi pichani kuhusiana na ziara ya ugeni huo wa Utalii wa Afya.























Waandishi wa habari wakifuatilia kwa makini mazungumzo hayo
Aidha ziara hiyo ya Kitalii (Utalii wa afya) itafanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee kuanzia tarehe 30-31 August,2012 kwa lengo moja likiwa ni kujuana na wasomi na kuelimishana na kuboresha huduma.
MKUTANO WA KUNDI LA G77 NA CHINA  UNAENDELEA NCHINI CHINA











EVELYN MKOKOI
BANGKOK, THAILAND 
29/8/2012
MKUTANO WA KUNDI LA G77 NA CHINA UNAENDELEA

Mkutano wa mabadiloko ya tabia nchi unaendelea mjini Bangkok, ambapo leo
kundi la G77 na China limekutana kwa mara ya pili na kujadili mambo mbali mbali
ikiwa ni pamoja na kuangalia namna mpango wa kupunguza gasi joto duniani
utakavyoweza kufanya kazi.

Katika mkutano wa leo, kundi hilo limejadili pia namna ambavyo nchi
zinazoendelea zinapaswa kuainisha taarifa zinazohitajika katika kukabiliana na
mabadiliko ya tabaia nchi, ikiwa ni pamoja na mipango na masuala ya fedha,
teknolojia na taaluma.

Aidha, washiriki wamejadili kuhusu juhudi za pamoja za kukabiliana na
mabadiliko ya tabia nchi kwa ujumla na kuwa na hali ya kuweza kufikia malengo
ya pamoja ya kukabiliana na madhara yatokanayo na mabadiliko ya tabaia nchi.

Aidha, katika mkutano wa leo umesisitizwa umuhimu wa kila nchi kuwa ‘serious’
katika suala zima la kukabiliana na athari zitokanazo na mabadiliko ya tabianchi
ikiwa ni pamoja na kuchukua hatua sahihi ili kuweza kufikia malengo ya kuhimili
na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

Washiriki pia walitilia mkazo suala la technolojia linavyoweza kuchangia katika
athari za mabadiliko ya tabia nchi, na walipata nafasi ya kujadili kwa kifupi
kuhusu mkutano wa dunia (COP18) wa mabadiliko ya tabia nchi utakaofanyika
mjini Doha mwezi wa Disemba mwaka huu.

Monday, August 27, 2012

NAPE AIKOMALIA CHADEMA AKATAA KUOMBA RADHI











Akataa kuomba radhi, asema tuhuma atazithibitisha mahakamani, Amtaka Dk. Slaa kuandaa bilioni 3 na shilingi moja. Ni kwa kudai CCM inaingiza silaha nchini.

KATIBU wa Halmashauri Kuu ya Taifa Itikadi na Uenezi CCM, Nape Nnauye amewataka Chadema kwenda mahakamani haraka badala ya kusubiri kuombwa radhi kama walivyotaka ili kusafishwa dhidi ya madai ya chama chao kupewa mabilioni ya fedha na mataifa tajiri.

Aidha amemtaka Katibu Mkuu wa chama hicho Dk. Wilbrod Slaa kuiomba radhi CCM la sivyo itamburuza mahakamani kudai fidia ya sh. bilioni 3 na shilingi moja, kwa kuituhumu uongo kwamba imeingiza silaha kutoka nje ya nchi tena bila kulipia ushuru.

Nape alisema hayo leo Agosti 27, 2012, kwenye mkutano wake na waandishi wa habari, uliofanyika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, mtaa wa Lumumba mjini Dar es Salaam.

"Bila shaka mmesikia jana Chadema wakinitaka niombe radhi au wananipeleka mahakamani kudai fidia ya sh. bilioni 3, kwa madai eti nimesema Chama hicho kinapata mabilioni ya fedha kutoka kwa mataifa tajiri. Mkubwa hatishiwi nyau, nawataka waende haraka mahakamani wala wasisubiri hizo siku saba", alisema Nape.

Alisema, CCM inao ushahidi wa kutosha kuhusu madai aliyotoa Nape dhidi ya Chadema na kwamba huyo tayari kutoa uthibitisho huo mahakamani badala ya kuomba radhi.

"Nadhani wakienda mahakani itapendeza zaidi maana huko ndiko pazuri kutoa uthibitisho kuhusu tuliyosema, na ninawahakikishieni tukishathibitisha na Msajili wa Vyama akaupata uthibitisho huo chama chao kinafutwa", alisema.

Kuhusu CCM kumburuza Dk. Slaa mahakamani, Nape alisema, ameshawaagiza wanasheria wa Chama, kuandaa barua ya kusudio la mashitaka hayo, na Dk. Slaa atapelekewa ili aamue kama ataomba radhi au atakuwa tayari kwenda mahakamani.

"Wakati wanakwenda mahakamani, Chadema wamwambie babu yao ajiandae kuomba radhi au kuburuzwa mahakamani kuilipa CCM fidia ya sh. bilioni 3 na shilingi moja kwa kuizushia CCM uongo kwamba inaingiza silaha nchini tena", alisema Nape.
MWISHO.

Sunday, August 26, 2012

RAIS KIKWETE NA FAMILIA YAKE WAHESABIWA SENSA YA WATU NA MAKAZI
















Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Mkewe Mama Salma Kikwete na familia yake akijibu maswali toka kwa karani wa sensa ya watu na makazi Bw. Clement Ngaliba Agost 26,1012.(Picha na Ikulu)
























Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Mohamed Gharib Bilal akijibu maswali toka kwa karani wa sensa Happiness Masaka .
Viongozi hao wamejiunga na mamilion ya watanzania katika zoezi la kuhesabiwa litakalodumu kwa muda wa siku saba. ambapo zoezi hilo kwa jana lilianza kwa mafanikio makubwa.

Friday, August 24, 2012

LADY JAY DEE KUPAMBA SHOW YA REDD'S MISS ILALA 2012

























Mwanamziki mkongwe hapa nchini Lady Jay Dee katikati akiwa katika picha ya pamoja na warembo watakaowania taji la Redd's Miss Ilala 2012. (Habari zaidi tutawaletea wadau wetu)
WASANII NYOTA WA BONGO MOVIE WATUA MJI WA MOSHI KUWAKILISHA TAMASHA LA SERENGETI FIESTA LEO






































































Tamasha hilo linafanyika uwanja wa Chuo cha Ushirika ndani ya jiji la Moshi , ambapo bongo movie wapo hapo kwa shughuli za kusaka vipaji vipya mbalimbali vya filamu, Usahili huo unafanyika kwenye ukumbi wa Mr. Price ulioko mtaa wa Malindi.

Thursday, August 23, 2012

MKUTANO WA 14 WA MAWAZIRI WA MAZINGIRA AFRIKA KUFANYIKA ARUSHA MWEZI UJAO                                                                                                                                                   


























Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Rais Mhe. Sazi Salula akiongea na waandishi wa habari kuhusiana na mkutano huo.
Tanzania imepewa heshima ya kuwa mwenyeji wa mkutano huo kwa muda wa miaka miwili mfululizo kwa mwaka huu 2012 na 2013 , ambapo Mawaziri wa nchi za Afrika wanatarajia kuwasili hapo kuanzia Septemba 10 hadi 14 mwaka huu.
Akizungumza na waandishi wa habari Mkurugenzi wa Mazingira katika nchi za Afrika ambaye ndiye mratibu wa mkutano huo Bw. Mounkaila Goumandakoye , alisema utawashirikisha Mawaziri wa nchi za Afrika kwa kuzungumzia utunzaji wa mazingira na jinsi ya kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa yanayoikumba nchi za Afrika .
Mkutano huo unashirikisha zaidi ya watu 3000 ambao wote watakuja kuzungumzia swala hilo, ambapo mwenyekiti wa mkutano huo atakuwa Waziri wa Mazingira Ofisi ya Rais Mhe, Dkt . Tezezya Huvisa.
RAIS KAGAME WA RWANDA AIKARIBISHA YANGA IKULU YA KIGALI                                 
























Rais Paul Kagame wa Rwanda akisalimiana na mwenyekiti wa wa bodi ya wadhamini wa Yanga mama Fatma Karume, wakati alipowakaribisha mabingwa hao wa Kombe la Kagame 2012 Ikulu ya Kigali jana jioni.



Wednesday, August 22, 2012

MAKARANI 800 WAGOMA KULA KIAPO CHA SENSA


































MAANDALIZI ya Sensa ya Watu na Makazi inayotarajiwa kufanyika Agosti 26, mwaka huu yameingia dosari baada ya matukio kadhaa ya kukwamisha kazi hiyo kujitokeza katika mikoa mbalimbali, ukiwamo Dar es Salaam ambako zaidi ya makarani 800 wamegoma kula kiapo cha utii na kutunza siri.
Habari zilizopatikana jana zimeeleza kuwa mbali na makarani hao, vipeperushi vyenye ujumbe wa kutaka watu wagomee Sensa vimesambazwa mkoani Arusha, huku mkoani Tanga kukiwa na tukio la Sheikh mmoja kutiwa mbaroni kwa kusambaza vipeperushi vya aina hiyo.
Makarani hao waligoma jana ikiwa ni siku yao ya mwisho ya mafunzo ya kazi ya kuhesabu watu na makazi. Makarani hao kutoka vituo mbalimbali kulikotolewa mafunzo hayo, walisema wameamua kugomea kiapo hicho kutokana na fedha zilizotengwa kwa ajili ya malipo ya kazi hiyo kuchakachuliwa kinyume na makubaliano.
Baadhi ya vituo ambavyo makarani wake wamegoma ni Shule ya Sekondari Makumbusho, Kambangwa, Shule ya Msingi Zawadi na vituo kadhaa vilivyopo maeneo ya Buguruni na Kawe.Baadhi ya makarani hao walionekana wakiwa katika makundi, muda ambao walipaswa kuendelea na mafunzo yao kabla ya kula kiapo cha kushiriki Sensa kwa uaminifu na ukamilifu.Baadhi ya makarani ambao waliomba majina yao yasitajwe gazetini, walisema imekiuka makubaliano ya awali.

“Serikali imesema imetenga Sh141 bilioni kwa ajili ya Sensa. Sisi tayari tuliingia makubaliano nayo kwamba tunatakiwa kulipwa Sh35,000 kwa siku, kwa muda wa siku saba jambo ambalo limegeuka na kuwa kinyume.”

“Ukipiga mahesabu fedha ambazo tungetakiwa kulipwa kwa siku hizo saba ni Sh245,000 lakini wao wamekuja hapa na kutupa Sh140, 000 tu. Hatuwezi kuendelea na kazi mpaka tulipwe fedha zetu.”
Karani mmoja katika Kituo cha Sekondari ya Kambangwa, alisema wameamua kugomea kiapo baada ya kuona kuwa mpaka mafunzo yanahitimishwa jana, baadhi yao hawajalipwa chochote.

RC Dar:Watalipwa
Akizungumzia madai ya makarani hao, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadiki alisema mpaka jana mchana makarani wote walipaswa kulipwa awamu ya pili ya fedha zao. Alisema awamu ya kwanza ya malipo hayo ilifanywa katika siku tano za mwanzo.“Kuna watu wamejichomeka katika zoezi hili, lakini kama kweli karani ameteuliwa lazima atalipwa pesa zake na kama imetokea amesahaulika basi afanye mawasiliano na mratibu wa Sensa wilaya anayotoka ili alipwe,” alisema.

Sheikh mbaroni
Katika hatua nyingine Sheikh Juma Koosa (52) anashikiliwa na polisi wilayani Morogoro akituhumiwa kutumia kipaza sauti kuwatangazia wananchi wasishiriki Sensa.

Sheikh huyo ambaye pia ni mwanafunzi wa mwaka wa pili wa Chuo Kikuu cha Kiislamu Morogoro, alikamatwa Agosti 19 mwaka huu alipokuwa kwenye Msikiti wa Miembeni, Mazinde mara baada ya kukaribishwa na wenyeji wake kuzungumza.Imedaiwa kuwa Koosa alitoa kitabu chenye kueleza sababu za kuwakataza Waislamu kutokushiriki Sensa mwaka huu.

Tuesday, August 21, 2012

DK. DALALY KAFUMU AVULIWA UBUNGE JIMBO LA IGUNGA, MKOANI TABORA.
































Mahakama Kuu ya Kanda ya Tabora imetoa hukumu ya kesi ya ubunge iliyokuwa ikikmabili mshindi wa Ubunge jimbo la Igunga,DK. Dalaly Peter Kafumu (CCM). Hukumu hiyo ambayo ilikuwa ni ya kupinga matokeo yaliyompatia ushindi DK. Kafumu imetolewa leo ambapo imemuengua mbunge huyo katika nafasi yake ya ubunge .
Shauri hilo lilifunguliwa na mlalamikaji Joseph Kashindye ambaye alikuwa mgombea mwenzie dhidi ya Dk.Kafumu.

Saturday, August 18, 2012

SWALA YA EID EL FITR KITAIFA KUFANYIKA MKOANI RUVUMA.























Swala ya Eid El Fitr na Baraza la Eid Kiaifa mwaka huu vitafanyika Masjid L - huda Msikiti wa Bakwata Songea katika Mkoa wa Ruvuma. 
Aidha kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu wa Baraza Kuu la Waislam Tanzania Suleiman Lolila, Swala hiyo itafanyika kati ya tarehe 19 au 20 Agost 2012 kutegemea mwandamo wa mwezi.
Taarifa hiyo imefafanua kuwa Baraza la Eid litafanyika kati ya tarehe hizo kuanzia saa kumi kamili alasiri na Mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Mkuu wa Mkoa Ruvuma Mhe. Said Mwambungu.
RAIS DKT.JAKAYA KIKWETE NA RAIS JOYCE BANDA WA MALAWI WAKUTANA MSUMBIJI NA KUZUNGUMZIA MGOGORO WA MPAKA
 Rais Kikwete akutana na Rais Banda mjini Maputo,Msumbiji leo kuzungumzia kutafuta suluhu katika mgogoro wa mpaka kati ya nchi hizo mbili Tanzania na Mawali uliopo katika Ziwa Nyasa. Aidha nchi hizo zipo katika kutafuta suluhu kwa njia za Kidiplomasia kupitia kamati maalumu iliyoundwa kushughulikia mgogoro huo. picha na Freddy Maro.



WANANCHI WATAKIWA KUIBUA MIRADI YA MAENDELEO


Habari na Salma Mrisho, Geita
Wananchi wametakiwa kujua kwamba maendeleo hayawezi kuja bila wao kujitambua kuwa wana nafasi katika kushiriki na kutoa maoni katika kuibua miradi mbalimbali ya kijamii itakayowaletea maendeleo.
Hayo aliyasema Afisa mipango wilaya ya Geita mkoani Geita Bw Andrew Chikwanda alipokuwa akizungumza na mwandishi wa gazeti hili kuhusu uhusikaji wa wananchi katika uibuaji wa miradi.
Alisema kuwa wananchi,wadau na serikali ni watu wanaotegemeana katika shughuli mbalimbali hasa za kuibua miradi na kila mmoja kwa nafasi yake anatakiwa aisimamie kikamilifu ili matunda ya hiyo miradi ionekane.
“zamani serikali ilikuwa inatoa fedha na kuanzisha miradi lakini ilionekana ile miradi matokeo yake yalikuwa madogo na wakati mwingine ilikuwa haionekani  thamani ya miradi lakini kwa sasa wananchi wana nafasi ya kuibua miradi yao na wafanye hivyo”alisema Bw Chikwanda
Pia aliwataka wananchi kama walikuwa hawajui wana hiyo nafasi watambue na wakae katika vijiji vyao na waibue miradi ambapo inatakiwa ipitishwe na mkutano wa kijiji na mabaraza ya maendeleo ya kata na baada ya hapo wana kaa na madiwani na wataalamu kuijadili ipi ipewe kipaumbele kulingana na fedha iliyopo kwa mwaka husika.
Bw Chikwanda aliongeza kuwa miradi ya wananchi imekuwa na maendeleo kwa kuwa wao ndio waanzilishi na wanasimamia ipasavyo kuhakikisha inafanikiwa kuliko angefanya mtu mmoja ambapo ingeweza kuchukua muda kukamilika.
“unajua wananchi wajue kuwa wao ndio wahusika na wasisibiri ile ruzuku inayotolewa na serikali kupelekwa ngazi ya kijiji ndio ifanye kila kitu maendeleo yatachelewa sana waibue tu miradi sisi ni watekelezaji wa kufanikisha hilo”alisisitiza Bw Chikwanda
Aliongeza kuwa kuwa mara nyingi wanatembelea miradi iliyobuniwa na wananchi na kuangalia viwango vya ujenzi kama vinakidhi na wanatoa nyaraka kuwa kila hatua ya ujenzi ihakikishe nkuwa mhandisi ametoa  cheti  ili kuruhusu hatua nyingine iendelee.
Aidha aliwataka wakuu wa idara na ofisi ya ujenzi kutembelea miradi inayoanzishwa na kuoana thamani yake na hata kutoa ushauri kuliko kuacha miradi inaendelea na ikikamilika kuonekana kuna kasoro kwani kwa kufanya hivyo tutakuwa tunawaangusha wananchi kwa nguvu kazi zao walizotumia.

MWISHO

Wednesday, August 15, 2012


SENSA HAITAWAACHA WAFUGAJI WA GEITA
  
Habari na Salma Mrisho , Geita

Mkufunzi wa sensa ngazi ya Mkoa wa Geita Cosmas Kapinga amewahakikishia madiwani kuwa hakuna mtu yeyote atakayekosa kuhesabiwa katika zoezi la sensa hata akiwa porini.
Kauli yake hiyo ilikuja baada ya Diwani wa Kata ya Iyogero wilaya ya Bukombe katika semina ya madiwani kuhusu sensa ya watu na makazi kutaka kujua jinsi gani wafugaji watahesabiwa kwa kuwa wao wanahama maeneo kila siku.
Diwani huyo alidai kuwa hayupo kiongozi anayejua kuwa mfugaji yuko  wapi na hata kama uliwaona eneo lako ukiwafatilia siku nyingine wwanakuwa wameshahama kwa namana hiyo zoezi hili litakosa idadi ya wafugaji.
Akijibu swali hilo Bw  Kapinga alisema kuwa kwa upande wa wafugaji kutakuwa na karani wa sensa ambaye ataandamana na kiongozi wa sehemu husika kwenye maeneo yake na siku tatu kabla ya sensa karani atakua kehsayajua maeneo kwakua wanayatembelea kabla ya zoezi lenyewe.
“ndugu madiwani hilo lisiwatie shaka kabisa tuna ramani ya kila eneo na karani anayajua maeneo yake ya kazi kwani suala la wafugaji lisiwatie mashaka kabisa “alisema Kapinga
Pia aliwataka madiwani  muda uliobaki wawaelimishe wananchi juu ya umuhimu wa sensa hasa wafugaji wanaohamahama kila kukicha na wajue kuwa agosti 26 ndio zoezi lenyewe na ni muhimu kupata takwimu za wafugaji.
MWISHO


WANANCHI WA GEITA NA MATATIZO YA USAFIRI 

Habari na Salma Mrisho ,Geita .
Wananchi wametakiwa kuwa na subira katika mchakato unaoendelea wa kuhakikisha suala la usafiri linaboreshwa kuanzia mijini hadi vijijini.
Hayo yalisemwa na Mkuu wa Wilaya Manzie Mangochie  wakati wakizungumza na wadau mbalimbali mwishoni mwa wiki  juu ya kuboresha suala la usafiri wa abiria mkoani hapa.
Alisema kuwa wananchi walikuwa wanapata tabu juu ya usafiri hasa baada ya kupiga marufuku magari madogo aina ya michomoko iliyokuwa inabeba abiria wengi na ni kinyume cha sheria na kuongeza kuwa kwa sasa tatizo hilo limetatuliwa kwani wafanyabiashara wa  magari aina ya hiace wameyaleta kutoka mwanza  na yanatoa huduma ya usafiri.
“wananchi jamani muwe mnatupa taarifa sio mpaka ajali zitokee na kama kuna michomoko sehemu inafanya kazi mtujulishe sheria ichukue mkondo wake”alisema Manzie
Alisema kuwa kwa sasa wanajipanga ili waweze kuweka vituo kila eneo na ili Geita iendane na hadhi ya Mkoa kuliko ilivyo sasa usafiri wa baiskeli umekuwa mwingi na pikipiki na wataalamu wamepitia baadhi ya maeneo ambapo umbali wa mji kwa km 10 kuna ruti zishapangwa na kwa vigezo vya Sumatra nauli itakuwa shilingi 500.
Aidha aliwataka wananchi watoe taarifa juu ya madereva wanaovunja sheria barabarani ili kuzuia ajali zinazoweza kuepukika mkoani hapa.
Kwa upande wamkuu wa wa Kikosi Cha Barabarani Kamanda John Mfinanga aliwahakikishia wananchi kuwa watafatilia kwa karibu kero zote za usafiri na kuhakikisha magari hayajazi abiria wengi na sheria zinazingatiwa.

MWISHO

Tuesday, August 14, 2012

FAHARI YA TANZANIA : SEHEMU YA HIFADHI YA TAIFA YA ARUSHA...!

































































Monday, August 13, 2012

MSAMA PROMOTION WAKAMATA CD NA DVD FEKI ZA KAZI ZA WASANII ZILIZOINGIZWA SOKONI,JIJINI DAR ES SALAAM.



















Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion , Bw. Alex Msama akionyesha CD na DVD feki za kazi za wasanii zilizoingizwa sokoni zenye thamani ya Sh. Million 11 huko Mbagala Jijini Dar es Salaam.

Zoezi hili la kukamata CD na DVD hizo linaendeshwa na Kampuni hiyo kwa kushirikiana na Polisi , likiwa na lengo la kuwadhibiti wezi wa kazi hizo za wasanii nchini. 

Saturday, August 11, 2012


MSIMAMO WA MEDALI KATIKA MICHUANO YA OLYMPIC INAYOENDELEA HUKO UINGEREZA

Medal Table

Rank      Country Gold Silver Bronze Total
1 United States 41 26 27 94
2 China 37 25 19 81
3 Great Britain & N. Ireland 25 15 17 57
4 Russian Federation 15 21 27 63
5 South Korea 13 7 7 27
6 Germany 10 18 14 42
7 France 9 9 12 30
8 Hungary 8 4 3 15
9 Australia 7 14 10 31
10 Italy 7 6 8 21
11 Netherlands 6 5 8 19
12 Kazakhstan 6 0 4 10
13 Japan 5 14 16 35
14 Iran 4 5 1 10
15 New Zealand 4 3 5 12
16 North Korea 4 0 2 6
17 Jamaica 3 4 3 10
18 Cuba 3 3 4 10
18 Belarus 3 3 4 10
20 Ukraine 3 1 9 13
21 South Africa 3 1 1 5
22 Ethiopia 3 0 3 6
23 Spain 2 8 3 13
24 Romania 2 5 2 9
25 Denmark 2 4 3 9
26 Kenya 2 3 3 8
26 Czech Republic 2 3 3 8
28 Brazil 2 2 8 12
29 Poland 2 2 6 10
30 Turkey 2 2 1 5